TUCHAGUENI TUBORESHE BANDARI YA MTWARA ZAIDI DKT. SAMIA

 

Mgombea wa Urais kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewaomba 

wananchi wa mkoa wa Mtwara wamchague ili serikali iendelee kuboresha na kupanua uwezo wa bandari ya Mtwara.


 Ameeleza kuwa maboresho 

yaliyofanyika tayari yameifanya bandari hiyo kuwa lango muhimu la biashara 

kwa ukanda wa kusini, na kwamba hatua zaidi zitachukuliwa ili mazao ya 

biashara kama korosho yasafirishwe moja kwa moja kutoka Mtwara kwenda 

masoko ya kimataifa. 

Dkt. Samia pia amesisitiza umuhimu wa bandari ya Mtwara kama kituo pekee 

kinachosafirisha makaa ya mawe nchini, jambo linaloiongezea nafasi kubwa 

katika uchumi wa taifa.

 Ameahidi kuwa endapo ataendelea kuongoza, 

serikali yake itawekeza katika miundombinu na huduma za bandari hiyo, 

sambamba na kurahisisha upatikanaji na usafirishaji wa pembejeo za kilimo 

kwa wakulima wa korosho.

Post a Comment

0 Comments