JESHI LA POLISI LAWAFUNDA WAANDISHI PWANI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani leo limeendesha mafunzo  ya siku moja kwa waandishi wa habari  wa Mkoani hapa yanayohusu  Wajibu na Usalama  wa Waandishi wa Habari  wakati wa uchaguzi  2025.

Akizungumza  na waandishi hao kwenye mafunzo yaliyofanyika  kwenye Ukumbi wa mikutano  uliopo  kwenye jengo la Polisi Mkoa wa Pwani RPC  Salim Morcace amewasisitiza wana habari kuchakata taarifa zenye tija, weledi  na uzalendo  kwa sababu vyombo vya habari wanalo jukumu la kulinda  amani ya nchi.

"Wajibu wa Jeshi  la Polisi  katika  kulinda  usalama  wakati wa uchaguzi  uwepo wa Jeshi la  Polisi Tanzania ni kwa mujibu  wa sheria  mama yaani  katiba  ibara ya 147(4), Kuhusu uundwaji /uanzishwaji  wa Majeshi  ya Ulinzi na Usalama" amesema RPC Morcace. 

"Jeshi la polisi lina jukumu la kulinda  maisha na mali za wananchi  kubaini ,kuzuia  na kutanzua uhalifu,kupeleleza,kuhifadhi  ushahidi na kukamata" amesisitiza RPC Morcace. 

Akiwasilisha mada hiyo Kamanda Morcase amewasisitiza Waandishi  wa Habari Mkoa wa Pwani kuweka mbele  maslahi ya umma  ikiwa ni pamoja na kuandika habari kwa kutanguliza uzalendo  katika kulinda  na kuendeleza ustawi wa umma.

SSP  Elias Haway ametoa rai kwa Waandishi  kuepuka  kubashiri  matokeo ya uchaguzi, kueneza taarifa za  uvumi ,kupendelea na kuripoti madai  yasiyothibitishwa  ama  yaliyochakatwa  makusudi  kwa nia ovu kwa kutumia  teknolojia  ya  kidigiti.

"Vyombo vya habari  viepuke  kurusha  au kuchapisha  matangazo  ya kampeni ujumbe  wa kumuunga  mkono  mgombea au kuchakata maudhui  yoyote ya  kisiasa yenye  muelekeo wa kampeni  kwenye  magazeti  ,redio, televisheni,  na majukwaa ya kidigiti pale inapofikia ukomo wa kampeni  kwa mujibu wa Tume Huru ya Uchaguzi INEC".

"Vyombo vya habari havitaruhusiwa kuwa na vituo vya kujumlisha  matokeo  na badala  yake  vitapaswa kuripoti  matokeo rasmi ya uchaguzi kutoka kwenye Tume Huru ya Uchaguzi INEC   amesema SSP Haway.

Aidha SSP Ibrahim Nkindwa amesisitiza Waandishi  wazingatie usalama wao kwanza  pamoja  na wengine  ambao ni wanajamii tupeane elimu lipi ndilo na lipi halistahili.

"Epukeni kupokea rushwa ili kuandika habari za kupendelea upande fulani kwani Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU wako kazini.

Wakati huohuo SSP Nemes Kavishe  Mkuu wa Kikosi Cha Kutuliza Ghasia

Mkoa wa Pwani amesema kuwa anatoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika kushiriki Uchaguzi Mkuu  ujao uliopangwa kufanyika tarehe 29, Oktoba 2025 kwa utulivu na amani sambamba na kutii sheria bila shuruti .

"Haki bila wajibu haviendi sambamba"amesema SSP Kavishe.

 Mkaguzi  wa Polisi   Jesca Mwaikugile ambaye pia ni Afisa Habari wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani.

 INSP Mwaikugile amesisitiza kuwa  Jeshi hilo litaendelea kufanya kazi na Waandishi  wa Habari  ambao wataripoti habari  za uchaguzi ni wale ambao  wamepata  Ithibati  kutoka Bodi ya JAB ambao ni waandishi wa muda, waajiriwa wa kudumu na wanafunzi  ambao wanafanya mafunzo  kwa vitendo watakao pangiwa kazi  kipindi cha uchaguzi.

ASP Mwaikugile  amesisitiza waandishi kutovaa mavazi yenye kuashiria itikadi ya chama chochote cha siasa kwani ni kinyume na taaluma ya habari.

Mafunzo hayo yameshirikisha Waandishi wa Habari  kutoka vyombo mbalimbali vya habari Mkoani  Pwani.

Waandishi hao wameaswa kutoandika habari  kwa mihemko ya ushabiki  na shauku kupita kiasi ,kutokuandika habari ambayo haijakamilisha pande mbili zinazohusika ,kukwepa  kuandika habari  zenye upendeleo  na kujikita kishabiki.

Post a Comment

0 Comments