DStv YAZINDUA PROMOSHENI YA KUSISIMUA ONJA UTAMU WA JUU

Multichoice Tanzania kuwapa wateja nafasi ya “Kuonja Utamu wa Mitanange ya FIFA” kwa Kifurushi cha POA

Kampeni hiyo imezinduliwa  leo Jijini Dar es Salaam tarehe  16, 2025 ambapo  Kampuni ya Multichoice Tanzania, kupitia huduma yake ya DStv, imethibitisha dhamira yake ya kuendelea kuwa karibu na wateja wake kwa kuzindua kampeni mpya inayojulikana kama "Onja Utamu wa Mitanange", ikilenga kuwawezesha wateja kushuhudia michuano mikubwa ya FIFA kwa bei nafuu.

Akizungumza mapema leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Masoko wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo, amesema kampeni hiyo inalenga kutoa fursa kwa kila Mtanzania, hasa wapenzi wa michezo, kupata uhondo wa michuano hiyo mikubwa duniani 'LIVE' itakayopatikana kwa  kupitia kifurushi cha bei ya chini kabisa cha POA.

“Tunatambua umuhimu wa burudani ya michezo kwa wateja wetu. Kupitia kampeni ya 'Onja Utamu', sasa mteja yeyote akilipia kuanzia kifurushi cha POA, atapata nafasi ya kujionea mechi zote za michuano ya FIFA moja kwa moja, bila kulazimika kubadilisha kifurushi,” amesema Shelukindo.

Amesema  kuwa lengo kuu ni kuhakikisha hakuna Mtanzania anayekosa kushuhudia burudani hiyo ya kipekee, huku amesisitiza  kwa kusema kuwa Multichoice Tanzania itaendelea kuwekeza katika kuhakikisha itatoa huduma bora na zenye thamani kwa wateja wake na  zinapatikana kwa kila mtu  bila kujali uwezo wa kifedha.

Kutoka kushoto ni Kaimu Mkuu wa Thamani kwa wateja DSTV  Irene  Mwakijangala na Mkuu wa Masoko Multichoice Tanzania  Ronald Shelukindo.
Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa Dstv wakati wa hafla ya uzinduzi wa camapaign ya Promosheni Kabambe ya “Onja Utamu wa Juu”!  Iliyofanyikia katika makao makuu ya Dstv

Kampeni ya “Onja Utamu wa Mitanange” inakuja wakati ambapo mashabiki wa soka duniani kote wakiwa na hamasa kubwa kuelekea michuano hiyo mikubwa ya FIFA, na hivyo kuwa fursa adhimu kwa familia, marafiki na majirani kukusanyika pamoja na kufurahia burudani kupitia DStv.

Post a Comment

0 Comments