Dkt.Zhang alikuwa daktari Bingwa wa Dawa za Usingizi na Ganzi (Anesthesiologist), raia wa China aliyekuwa anafanya kazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Dkt.Zhang alikua na shahada ya udaktari wa binadamu (Bachelor of Medicine) Shahada ya upasuaji (Bachelor of Surgery), shahada ya umahiri katika matibabu ya ndani (Master of Internal Medicine) na shahada ya umahiri katika dawa za usingizi (Master of anesthesiology). Pia alikua na cheti cha ithibati ya kimataifa cha kuhudumu kama daktari bingwa wa dawa za usingizi katika nchi zaidi ya 100 duniani (NMLE).
Dkt. Zhang atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa wa kuhudumia jamii ya watanzania, pamoja na umahiri wake kufundisha njia mpya za dawa za usingizi na ganzi. Atakumbukwa pia kwa ucheshi wake, uchangamfu wake na passion yake katika kazi.
Dkt. Zhang amekufa kishujaa akijaribu kuokoa maisha ya Mtanzania mwenzetu aliyekua akizama.
Binti yake alimuona mwanamke wa kitanzania akitapata baada ya kuzama majini wakati anaogolea kisha akamwambia baba yake. Baba yake alijitosa kwenda kumwokoa mwanamke huyo.
Muhimbili. Dkt. Zhang ameacha mjane na watoto wawili wa kike.
Wapili kutoka kushoto ni mke wa Dkt. Zhang akilia kwa uchungu mara baada ya kuwasili nchini kushiriki mazishi ya mume wakeambapo mwili wake utachomwa moto siku ya Ijumaa Jijini Dar es Salaam.


0 Comments