Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), imesema waandishi wa habari ambao wataghushi vyeti na kuvitumia katika mfumo mpya wa kidigitali wakigundulika watachukuliwa hatua hali za kisheria ikiwa ni pamoja na kufunguliwa kesi ya jina na kufungiwa.
Mwenyeti wa JAB Tido Mhando amesema hayo leo tarehe 19 Mei 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za JAB zilizopo Jijini Dar es Salaam na kusema mfumo wa JAB ambao unajulikana kama TAI-HABARI una uwezo wa kubaini vyeti feki hivyo ni vema mwandishi kabla hajaweka cheti chake ajiridhidhe kwanza kwa kukihakiki.
"Tumepata taarifa kuwa kuna vyuo vinatumika kutoa vyeti vya kughushi na wote watakaofanya hivyo kwa uchu wa kupata fedha nasema wazi kuwa tutakuwa wakali kwani tutafuatilia taarifa zako katika mamlaka husika hata kama mmeanza kujipitisha kwenye vyuo hivyo ndani ya miezi miwili ili kuhalalisha kununua vyeti vya kitaaluma tutawabaini kwa njia tutakazo zitumia sisi", amesema, Mhando.
Mhando amesema waombaji lazima wazingatie vyeti ni halali na vimehakikiwa na mamlaka husika,ikwa pamoja na TCU na NACTVET mamlaka hizo ndizo zitatoa taarifa sahihi ili kuepusha usumbufu ,pia picha ya muombaji na taarifa zake ziwe za karibuni", amesema
Kwa mujibu wa kanuni ya 17(a) ya kanuni za sheria ya huduma za habari watu wanaopaswa kujisajili ili kuthibitishwa na kupatiwa vitambulisho ni wahariri,waandishi wa kujitegemea,watangazaji, wapigapicha wa vipindi vya habari, wanafunzi wa vyuo vya uandishi wa habari wanaokwenda mafunzo kwa vitendo na waandishi wa habari wa kigeni.
"Ili kujisajili katika mfumo wa TAI -HABARI mwombaji anatakiwa na namba ya simu na barua pepe vinavyofanya kazi ,picha ndogo ambayo haijaskaniwa, vyeti vya elimu vilivyo sainiwa, barua ya utambulisho kutoka katika taasisi anayotoka au anakopeleka kazi zake ikiwa ni mwandishi wa kujitegemea atahitajika kutuma nakala ya kitambulisho chake cha taifa NIDA na ada ya JAB ni 50,000 na Dola 500 kwa wandishi kutoka nje ya nchi ambayo itadumu kwa muda wa miaka miwili", amesema.
Mhando amesisitiza kuwa mahitaji haya ni muhimu ili kukamilisha mchakato wa maombi kwa mafanikio.
Amesema waaandishi wanapaswa kuingia kwenye kiunganishicha https//taihabari.jab.go.tz na kufuata maelekezo ya kujisajili.
Mhando amesema kuwa baada ya kujaza taarifa kwa usahihi mwombaji atapokea neno siri (code) kupitia SMS na barua pepe ili kuendelea na hatua za kujaza wasifu, kufanya maombi,kupata ankara ya malipo, kulipia na kuwasilisha maombi ya kupata kitambulisho (Press Card).
Mhando amesema kitambulisho cha Bodi (Press Card) kitatumika mahali popote ambapokutakua na shughuli za kihabari zinafanyika na mahali popote ambapo mwandishi wa habari anataka kufanya kazi ya kutafuta habari isipokuwa maeneo maalum yaliyozuiliwa kisheria.
Bodi ya Ithibati JAB ilizinduliwa Machi 3, 2025 na Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Prof.Palamagamba Kabudi Jijini Dar es Salaam.
Wakati huo huo Mhando amesema kuwa JAB inamipango endelevu kwa wandishi wa habari kwa sababu watakua na mfuko wa mafunzo ambao utakua na lengo la kuwaendeleza kitaaluma na kuwajengea uwezo, kukuza maudhui pia wamejipanga kuanzisha kituo ambacho kitakua huru na rafiki kwa waandishi wa habari watakaokuwa wanachama wa JAB ikiwa ni pamoja kuwakutanisha na kubadilishana mawazo sambamba na kufanya kazi zao.
Amesisitiza kua JAB ni mwamvuli wa kutetea haki za wanahabari pale watakapokumbana na changamoto katika kazi zao za kila siku kuwalinda na vitisho na manyanyaso yatakayojitokeza wakiwa kazini.



0 Comments