UWANJA WA SHIRIKA LA ELIMU KIBAHA KUTUMIKA MICHUANO YA CHAN ,AFCON 2025-27

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  amefanya ukaguzi wa Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha Mkoani Pwani ambapo utatumiwa kufanyia sherehe  za kuwasha Mwenge wa Uhuru   na kusema ameridhishwa na maandalizi aliyoyaona ikiwa ni ,jukwaa kuu mzunguko na watoto  watakaocheza halaiki.

 Waziri Mkuu amesema  hayo leo tarehe 30 Machi 2025 alipofika kukagua maendeleo ya maandalizi ya Uwanja huo kwa ajili ya sherehe za kuwasha Mwenge wa Uhuru  zitakazofanyika tarehe 2 Aprili 2025 ambapo ameonesha shauku  ya kuuboresha  zaidi Uwanja huo ili ukidhi vigezo  vya timu zitakazoshiriki katika Michuano ya  CHAN 2025 na AFCON 2027.

"Jana nimefanya ukaguzi Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF) kufanya tathmini ya kazi ya ujenzi na ukarabati wa viwanja vya mazoezi vitakavyotumika kwenye michuano  ya CHAN na AFCON  viwanja ni vichache ila baada ya kufika hapa nimeridhishwa na hali ya Uwanja huu kwani una kidhi vigezo vyote vya kuleta timu zije kufanya  mazoezi na hata mechi za Ligi Kuu Bara zinaweza kuchezwa katika Uwanja huu wa Shirika la Elimu Kibaha"

"Changamoto kubwa niliyoiona ni sehemu ya kuchezea (pitch) hii tutaitengeneza kwa kufukia madimbwi na kuusawazisha Uwanja , vyumba ya wachezaji (dressing rooms)  pia ikumbukwe timu ikija kukufanya mazoezi Kibaha wachezaji watalala kwenye Hoteli za hapa hivyo tutaingiza fedha za kigeni.

Tayari Waziri Mkuu Majaliwa amekagua  viwanja vya Gymkhana, Meja Generali Isamunyo na kiwanja cha Chuo cha Sheria(Law School ) kilichopo Simu 2000 Ubungo Jijini Dar es Salaam.

Michuano ya CHAN 2025 inayoshirikisha wachezaji wa ndani inatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 2 hadi 30 Agosti 2025 baada ya kuahirishwa mwaka 2024, Vilevile michuano ya Afcon inatarajiwa kufanyika mwaka 2027.

Akizungumza  kuhusu maandalizi  ya uzinduzi wa kuwashwa  Mwenge  wa Uhuru ambayo yamefikia asilimia 96 huku Mgeni Rasmi atakuwa Makamu wa Rais Dkt Philip Isdor Mpango.

Wakati huohuo amewatembelea vijana wanaocheza halaiki na kuwaahidi vifaa vyote wanavyotumia  wakati wa mazoezi na waalavyotumia siku ya kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru ni vya kwao na asitokee mtu wa kuwanyang'anya.


 

Post a Comment

0 Comments