Benki ya NMB imeungana na kusherehekea pamoja katika kilele cha siku ya Wanawake Duniani kwa kutoa michango ya madawati 100 na vitanda20 kwa Shule na mabati 100 kwa ajili ya kuezeka Zahanati Wilayani Mkuranga.
Akikabidhi Madiwati kwa Mkuu wa Wilaya Mkuranga Meneja wa Kanda Dar es Salaam na Pwani Seka Urio amemkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Khadija Nasri madawati 100 ambapo madawati 50 yatapelekwa Shule ya Kisemvule ,madawati 25 Shuke ya Msingi Chatembo na madawati mengine 25 yatapelekwa Shule Msingi Chatembo.
"Tunayoheshima kubwa sana kushiriki kwenye maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Wanawake 2025" amesema Urio.
Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kisemvule tarehe 8 Machi 2025 ambako ndiko kumefanyika maadhimisho ya sherehe hizo kimkoa.
Akizungumza kwa niaba Mkuu wa Mkoa wa Pani Alhaji Abubakari Kunenge, Mbunge wa Viti Maalum Chama Cha Mapinduzi (CCM),
Mh.Subira Mgalu amewaeleza wanawake waliofika kwenye sherehe hizo kuhakikisha ifikapo wakati wa uchaguzi mkuu wa 2025 wanamchagua tena Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa awamu nyingine tena.
"Twendeni tukampe kura za ndiyo kwa sababu hakuna mtu yeyote mwenye uwezo wa kuzuia uchaguzi mkuu hilo liko wazi"
amesema Mgalu.
Sherehe hizo zimepambwa na wahudhuriaji kutoka Taasisi mbalimbali ikiwa ni pamoja na TAKUKURU, PSSSF, NMB,CRDB, JKT RUVU, Mtandao wa Askari wa Jeshi la Polisi Pwani Shirika la Elimu Kibaha, Nyumbu,Wajasiriamali wote ndani ya Mkoa wa Pwani ambao walipata fursa ya kunesha bidhaa zao na wengineo wengi.





0 Comments