UWAMIZ WACHANGIA BENKI YA DAMU


Umoja wa Wajasiriamali zaidi ya 70 wa Mtaa wa Zigua na Mahiwa Kariakoo maeneo ya Msikiti wa Mtoro wamejitolea damu kwaajili ya maandalizi ya kuingilia mwezi mtukufu wa Ramadhani ikiwa ni mwezi 28 Shaaban1446 AH kwa lengo la kuchangia Banki ya damu salama ya taifa.
Yamesemwa hayo leo Februari  28 na Katibu wa Umoja wa Wafanyabiashara katika Mitaa ya Mahiwa  na Zigua Simba Issa Lichanda
Akizungumza  kabla ya kuanza zoezi  la utoaji wa damu.
Wakati zoezi la kuchangia damu likiendelea wafanyabiashara wengine nao waliendelea na kazi zao.
Imamu  Mkuu wa Msikiti wa Kwamtoro Ramadhan Abbas uliopo kati ya mitaa ya Mahiwa na Zigua  amesema kuwa  kutoa damu kwa hiari ni jambo la ibada katika imani huku akitoa wito kwa waumini wake kujitoa kwa ajili ya sadaka hiyo ambayo itawafaa wengine wenye uhitaji kama kima mama wajawazito na wagonjwa wengine walioko mahospitalini wenye kuhitaji  damu.
Imamu  Abbas  amesisitiza kwa kusema kuwa  uhutaji wa damu ni damu ya mwanaadamu na kamwe haiwezi kuwa na mbadala wake huku amewasisita wafanyabiashara  hao kuendelea  kutoa sadaka hiyo.
Afisa kutoka Kitengo cha Damu Salama  Adam. Kweka amesema kuwa  anawapongeza  waumini  wa dini ya Kiislamu kwa sababu wamekuwa  mstari wa mbele na wana rekodi ya kuongoza kwa uchangiaji wa damu nchini .

"Nawapongeza  ninyi mnawito na takwimu  zenu za uchangiaji zipo kwenye benki ya damu" amesema.

Pia nachukua fursa hii kutoa pongezi zangu kwa UWAMZ kwa kuhamasishana na kujitokeza kwa wingi katika kuchangia damu  kwani duniani hakujawahi kuwa na mbadala wa amu ieleweke hivyo.
Wanachama wa UAWAMZ waliendelea  na taratibu za  kutoa damu .Wakati huohuo
Mwenyekiti  wa Mtaa huo  Nasra  
Mohammed amesema kuwa anatoa wito kwa  wakaazi  na waafanya biashara  wote walioko hata nje ya mitaa hiyo ya Zigua na Mahiwa kujitokeza kuchangia damu kwani hakuna aijuaye kesho yake.

Post a Comment

0 Comments