TAMASHA LA KIZIMKAZI LAFIKIA TAMATI

Shamrashara za kusherehekea tamasha la Kizimkazi lililofanyika katika uwanja wa Mwehe Kusini Unguja.
Wasanii wakitoa burudani  kwenye tamasha hilo la kiutamaduni  kwenye Uwanja wa Mwehe Kizimkazi Kusini Unguja .
Shamrashamra  za kilele cha tamasha la Kizimkazi zikiendelea.
Baadhi ya wageni  waalikwa wakiwa katika kilele cha tamasha la Kizimkazi Uwanja wa  Mwehe  Kusini Unguja.
Kutoka kushoto  ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Isdor Mpango anayefuata ni msanii Hamonise,Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan  na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi wakifurahia jambo katika kilele cha tamasha la Kizimkazi  kwenye Uwanja wa  Mwehe Kusini Unguja. 
Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.
Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ahutubia Wananchi wakati wa Kilele cha Tamasha la Kizimkazi lililofanyika katika Uwanja wa Mwehe, Kusini Unguja Zanzibar.

Rais Dkt.Samia amesema kuwa kutokana na tamasha hilo kuwa namvuto zaidi kutajengwa   Uwanja  wa kisasa na utakaotumika katika michuano ya Afcon utakaokuwa na uwezo kuchukua watu 20,000 na uwanja huo unatarajiwa kuwa na viwango vya kimataifa  utakuwa na uwanja wa mpira wa miguu, netball,  basketball  na  viwanja vya michezo mbalimbali ikiwemo kuogelea pia kutakuwa na sehemu ya mapumziko na uwanja wa michezo ya  watoto ili kuwajengea watoto afya ya akili unatarajiwa kukamilika mapema mwakani  na ujenzi wake umetoka kwa CRDB Foundation na wapenda michezo. 

Post a Comment

0 Comments