KIBAHA KUANZISHA KILIMO CHA MBOGAMBOGA NA MATUNDA 

Waziri  wa Wizara ya Kilimo Mhe. Daniel Chongolo (Mb) amesema kuwa Mkoa  wa Pwani utaanza  kilimo  cha mbogamboga na matunda  kitakachoanza hivi karibuni katika eneo lenye ukubwa wa  eka 200 .

Akizungumza  leo  tarehe 16 Machi 2026   wakati akikagua eneo hilo lililopo Ruvu Stesheni Kibaha Vijijini  Mkoani Pwani amesema kuwa  ameridhishwa  na mandhari hayo  na  kusisitiza  kuwa kilimo hicho cha mbogamboga na matunda  kitazalisha ajira kwa vijana wa Wilaya ya Kibaha na Dar es Salaam pamoja na wananchi wanaoishi katika maeneo ya jirani .

"Mahitaji ya mbogamboga na matunda   ni makubwa  hivyo shamba hili litasimamiwa na wataalamu  wetu ambao wataelekeza walimaji kilimo cha kisasa  ili kiwe chenye ufanisi na kuleta tija ambapo Kibaha  itaillisha Dar es Salaam  na Zanzibar kwa matunda na mbogamboga" amesema Mhe.Chongolo.


Wakati huo huo  Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge  amesema kuwa hiki kitakuwa killimo cha muda mfupi na chenye tija kwa jamii ambapo 

leo tumekuja kufanya tathmini  ya eneo hili ambalo kilimo kitafanyika kisasa na kitakuwa cha kipindi cha mwaka mzima  bila kutegemea mvua sababu tunayo miundombinu  ya kumwagilia maji safi     na eneo  hili litaanza kusafishwa mara moja  ikiwa ni katika  hatua za awali za kuandaa shamba kwa kufuata maelekezo  kutoka kwa wataalamu wetu


 

Post a Comment

0 Comments