"KAMA JINA LA FILBERT BAYI LINAWAKWAZA LIONDOLEWE "BAYI

Baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha nne katika Sekondari ya Filbert Bayi iliyopo Mkuza Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.
Kaimu Mkurugenzi Fedha na Utawala Chuo Cha Diplomasia Jacob Nduye akikabidhi cheti kwa mmoja ya mwanafunzi kwenye mahafali hayo. 
Baadhi ya Wahitimu wa darasa la saba kutoka Shule ya Msingi Filbert Bayi yenye mchepuo wa Kiingereza  za Kimara na Mkuza.
Mgeni rasmi katika mahafali hayo Kaimu Mkurugenzi Fedha na Utawala Chuo Cha Diplomasia Jacob Nduye akimkabidhi cheti mwanafunzi wa kidato cha nne kwenye mahafali  ya Shule ya Filbert Bayi. 

MEJA Mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania  (JWTZ) ambaye pia alikua mwanariadha aliyeng'ara  katika medani ya mchezo wa riadha Olympic  mwaka 1974 Filbert Bayi pichani juu  amesema kuwa Shule yake inakabiliwa na changamoto  ya miundombinu ya barabara. 

Tangu nianzishe Shule hii ya Filbert Bayi  changamoto  kubwa tunayo kumbana nayo ni barabara  kupitika kwa taabu.

"Inafika wakati natamani kusema kama tatizo ni hili jina langu ndiyo linasababisha hii barabara  kutotengenezwa  basi waliondoe huenda kuna watu linawakwaza lakini wakumbuke  hii siyo njia yangu binafsi huku kuna wanafunzi ambao wanapitiwa  kutoka Shule  tofauti ,wanajeshi na wananchi wa kawaida wote wanatumia njii hii" amesema  Bayi.

 Meja Mstaafu  Bayi amesema hayo Agosti 24 katika mahafali ya darasa la saba  ya Shule ya Msingi Filbert Bayi iliyopo Kimara na Shule ya Msingi na  wanafunzi wa Kidato cha nne  wanaosoma  Shule ya Filbert Bayi iliyopo Mkuza Wilayani Kibaha Mkoani Pwani. 

"Nimesha fanya jitihada binafsi miaka yote tangu Shule  hii ilipoanza 2006 hadi sasa ikiwa ni pamoja na kuweka mawe kwenye barabara  kuchonga kwa kupitisha greda lakini sasa hivi nimechoka  sababu hii siyo njia yangu binafsi" amesema Bayi.

Bayi ameongeza kwa kusema kuwa mbona zipo barabara  nyingi za watu mashuhuri nyingi zinafanyiwa matengenezo  kwanini hii yenye jina la Filbert  Bayi  haithaminiwi?amehoji Mwanariadha aliyevunja rekodi ya Olympic   na Meja Mstaafu wa JWTZ. 

Bayi ameongeza  kwa kusema kuwa  Kamati ya Bunge ambao walitembelea Shuleni  hapo hivi karibuni walikwama kwenye barabara  hiyo na wakampigia simu Meneja TARURA, anashukuru wananchi wamepaza sauti zao TARURA wamemwaga kifusi na kusisitiza  wajitahidi kufanya matengenezo katika barabara  hivyo kwani  utabiri wa hali ya hewa  wametoa tahadhari kuna mvua zitanyesha hivi karibuni.
 Mgeni rasmi  katika mahafali  hayo Kaimu Mkurugenzi  Fedha na Utawala  Chuo Cha Diplomasia Jacob Nduye amewaasa wanafunzi waliohitimu  kuishi kwa kumtanguliza Mungu, kuwa na heshima na utii na kuzidisha juhudi ya msingi bora waliopatiwa shuleni  hapo sambamba  na kuendeleza sofa njema ya Shule hiyo kwani kuna rekodi ya wanafunzi waliohitimu shuleni hapo wengi wamepata nafasi nzuri katika ngazi za serikali  na sekta mbalimbali. 
Bayi anashikilia rekodi ya kukimbia  KM1500 katika michezo ya Jumuia ya Madola ya mwaka 1974 aliposhinda  Medali ya dhahabu.
   
Aidha Filbert Bayi  ni Katibu  Mkuu wa  Kamati ya Olimpiki ya Tanzania  (TOC) na hivi karibuni Agosti 6 mwaka huu amepewa heshima  ya kuwa miongoni mwa wanariadha nyota waliovunja rekodi za dunia. ambapo Rais wa Shirikisho la  Riadha Duniani Lord Sebastian Coe ndiyo aliandaa hafla  hiyo na Bayi amejumuishwa rasmi kwenye  jumba la Makumbusho  la wanariadha nguli  Duniani  iliyopo Jijini Paris nchini Ufaransa.
Mgeni rasmi kwenye Mahafali hayo Kaimu Mkurugenzi  wa Fedha  na Utawala Chuo Cha Diplomasia Jacob Nduye  kilichopo Kurasini Jijini Dar es Salaam akizungumza na wahitimu hao pamoja na wazazi kwenye mahafali hayo.

Post a Comment

0 Comments