CHALINZE MODERN ISLAMIC WAFANYA ZIARA YA KIMAFUNZO HOSPITALI YA RUFAA TUMBI


Conversatio
Wanafunzi hao wakiwa katika picha na mwalimu wao wa somo la Sayansi Rashid Hamis Stambuli

Muuguzi wa zamu kitengo cha kusafisha figo Joyce Mfyuji akiwaelekeza jambo wanafunzi hao

Dkt bingwa wa watoto wadogo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Pius Muzzazi


Wanafunzi hao wakiwa katika picha ya pamoja na muuguzi wa wodi ya watoto

WANAFUNZI  wa Shule ya Msingi  Mchepuo wa Kiingereza ya Chalinze Modern Islamic wamefanya ziara ya  masomo kwa siku moja  na kujifunza mambo mbalimbali. 

Akizungumza  kwa niaba ya wanafunzi hao Mwalimu wa Somo la Sayansi  Rashid Hamisi Stambuli amesema  kuwa  wanaushukuru uongozi  wa Hospitali ya rufaa Tumbi  Mkoa wa Pwani kwa kuwapa fursa wanafunzi hao ambao  ni Madaktari Tarajai kwani wameweza kutimiza lengo letu  kwa asilimia 99% katika masomo ya Sayansi wanayosoma  shuleni  hapo.

"Hii ni mara ya  ya kwanza  Shule  yetu kupata nafasi ya kupata ziara ya kimafunzo kwa  vitendo wanafunzi wetu wenye ari ya kuja kuwa madaktari wetu wa baadaye wametembelea idara tatu ambazo ni Dharura, Idara ya kuchuja Figo na Wodi  ya Watoto kuanzia   umri wa siku sifuri hadi siku 28.

Akizungumza  na wanafunzi hao  Daktari Bingwa  wa Watoto wadogo Katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi  Dkt.  Pius Muzzazi  amebainisha kuwa miongoni mwa magonjwa yanayowaathiri watoto  wadogo ni kuwa ni  pamoja na kuwa na ukosefu wa afya ya akili unaosababishwa na  malezi  mabovu kutoka kwa baadhi  ya wazazi ikiwa ni pamoja na kuwafokea na kuwatolea kauli zisizofaa.

 "Watoto wengi wamekua wakipata msongo wa mawazo kutokana kupata maneno yasiyostahili kutoka  kwa watu wao wa karibu na  wanao wazunguka" amesema Dkt.Muzazzi.

Wakiwa katika ziara hiyo Muuguzi wa zamu   kitengo cha  kusafisha Figo  Joyce Mfyuji amesema kuwa jamii nzima inapaswa kubadili mtindo wa ulaji kwa sababu ndiyo chanzo kikubwa  cha kuharibu figo na kusisitiza kwamba endapo mtu ataupata ugonjwa huo itamlazimu  kuchuja figo kwa kusafisha damu  mara tatu kila wiki katika muda wote wa maisha yake. 

Mwanafunzi Mussa Swedi amezungumza kwa niaba ya wenzake  waliopata fursa katika ziara hiyo ya kimafunzo amesema kuwa  amejifunza kuwa siyo kila mgonjwa huwa anapelekwa moja kwa moja kwenye wodi  za watu maalumu (ICU),"nimejifunza  kwamba mgonjwa wa dharura anapofika hupokelewa na kupewa huduma pia nimejifunza mambo mbalimbali  ikiwa ni pamojana kutambua kuwa kiungo kinachoitwa figo ni muhimu sanakatika maisha ya binadamu hivyo watu wote  tunapaswa kukilinda kwa kuzingatia kula mko kamili, kufanya mazoezi.

"Pia nimefurahi kuonanamnamgonjwa akipatiwa huduma ya kusafisha damu hili limetujenga zaidi na kuona kaI ya Utabibu inahitaji uwe na moyo wa kujito zaidi"amesema Mussa.


Post a Comment

0 Comments