NSSF KUMWAGA NYUMBA YANGA



  Mkurugenzi   wa  uendeshaji NSSF , Crecentius Magori akizungumza.
KLABU ya yanga imeingia makubaliano ya kununua nyumba kwa ajili ya wachezaji wake  na  Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) .Akizungumza jana katika mkutano maalum na wachezaji hao Mkurugenzi   wa  uendeshaji NSSF , Crecentius Magori amewaambia wachezaji hao kijana mjanja mjini ni yule ambaye ana miliki nyumba ama ardhi kuliko magari huku akiwahamasisha wachezaji wa Yanga kuchangamkia ununuzi wa nyumba hizo ambazo ziko katika mradi wa makao mapya katika kijiji cha Dege Kigamboni jijini Dar es Salaam.

“Sisi tuko tayari kuwapa fomu  na kwenda kuwaonyesha nyumba hizo ambazo zimejengwa kisasa zaidi hivyo ningependa kuwashauri  pindi mnapopata fedha zenu za mikataba mkitoa kiasi ili kuweza kuwa kati ya wamiliki wa nyumba hizo” alisema Magori.

“Endapo utaweza kumudu na kutoa kiasi cha sh. mil.8  taslimu  na kulipa kwa miezi mitatu mfululizo unapewa NSSF wanamupa funguo  na kuendelea kulipa kila mwisho wa mwezi hadi kwa miaka 15 unakuwa mmiliki halali wa nyumba hiyo”alisema Magori.

Aidha aliongeza kwa kuwaambia wachezaji hao kwamba endapo utakufa ndugu anaweza kurithi nyumba hiyo.

Huku akiwasisitiza wachezaji ambao bado hawajajiunga na NSSF kufanya hivyo mara moja ili waweze kujivunia matunda ya uchezaji wa mpira hapo baadaye.

Wakati huohuo  Katibu wa Yanga  Beno Njovu aliwaambia waandishi wa habari kwamba hayo ni mawazo ya Mwenyekiti wa Yanga Yusuph Manji ambaye alizungumza na Mkurugenzi wa NSSF Ramadhan Dau ambapo wote kwa pamoja wameamua kuwawezesha wachezaji wa timu hiyo ili waweze kuwa na mali zao za kudumu hadi uzeeni.

Wavhezaji wa timu ya Yanga wakisikiliza kwa makini.

Post a Comment

0 Comments