Social Icons

Wednesday, December 5, 2012

SHAMSA FORD , MAYASA WARREJEA 'AFTER DEATH'


Shamsa Ford

Mayasa Mrisho 'Maya' katika pozi kabambe

BAADA ya kitambo kirefu cha mapumziko ya uzazi, msanii Shamsa Ford amerejea upya kwa kasi katika fani ya uigizaji akitarajiwa kuonekana kwenye filamu ya 'After Death' akishirikiana na wazoefu Mayasa Mrisho, Ruth Suka 'Mainda' na Jacklyne Wolper.
Shamsa aliyekuwa mmoja wa waigizaji waliofanya kazi kwa karibu na marehemu Steven Kanumba ameshiriki filamu hiyo iliyotayarishwa na Jacklyne Wolper kama njia ya kumuenzi Kanumba aliyefariki Aprili 6 mwaka huu.
Muongozaji wa filamu hiyo inayotarajiwa kuzinduliwa mapema mwakani. Leah Richard 'Lamata' alisema filamu hiyo mpya imemrejesha upya Shamsa na kukumbushia 'umoja' wa wasanii hao waliokuwa wakishiriki kazi na marehemu Kanumba.
"Ndani ya filamu yetu ya 'After Death' ambaye ni maalum kwa ajili ya kumuenzi Kanumba imemrejesha upya Shamsa Ford, aliyeigiza na akina Mayasa Mrisho 'Maya', Mainda, Irene Paul, Wolper, Patcho Mwamba na Uncle D aliyeigiza kama Kanumba."
Lamata, mmoja wa waongozaji wachache wa filamu wa kike nchini, mbali na wakongwe hao pia filamu hiyo imewashirikisha 'watoto wa Kanumba' Jenifer na Patrick na wanajipanga kwa ajili ya uzinduzi wake mapema mwakani.
"Tunapanga kuzindua mwakani katika ukumbi utakaotangazwa ambao siku hiyo itatumika pia kumkumbuka marehemu Steve Kanumba," alisema Lamata.
Lamata alisema mipango kwa ujumla juu ya uzinduzi huo utawekwa bayana kadri siku zitakavyokuwa zikisogea, ila alisisitiza utafanyikia jijini Dar es Salaam.

No comments:

 
 
Blogger Templates