LUDACRISS AWASILI DAR MAHSUSI KWA TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2011

  Muwakilishi wa Prime Time Promotions/Clouds Media Group,Balozi Kidamba akisalimiana na kumkaribisha mwanamuziki Ludacris,mara kwenye hoteli ya Kempinsk mara tu baada ya kuwasili jioni ya leo akitokea nchini Marekani.Picha Zote kwa hisani ya
Ahmad Issa Michuzi,
P.O BOX 4156,DAR ES SALAAM.
ww.michuzijr.blospot.com
Phone:0713 422 313/ 0783 422 313
Tanzania- East Africa.
 Muwakilishi wa Prime Time Promotions/Clouds Media Group,Balozi Kidamba akimuongoza Mwanamuziki Ludacris pamoja na watu wake kwenye hoteli aliyofikia -Kempinsk jioni ya leo mara baada ya kuwasili jijini Dar tayari kwa kukamua onesho lake moja ndani ya viwanja vya Lidaz Club jijini Dar.
  Ludacris akijiweka sawa kwa ajili ya kurekodiwa na Wana Wa Clouds TV jioni ya leo.
  Muwakilishi kutoka Prime Time Promotions/Clouds Media Group,Balozi Kidamba akiwafafanulia jambo Wageni aliokuja nao Mwanamuziki Ludacris jioni ya leo akitokea nchini Marekani.
 Mwanamuziki mahiri wa miondoko ya Hip Hop,ambaye pia ni muigizaji wa Filamu ajulikanae kwa jina la Christopher Bryian Bridges a.k.a Ludacris akiwasili leo jioni kwenye uwanja wa ndege wa Mwal Jk Nyerere na kupokelewa na Wenyeji wake.Mwanamuziki huyo ambaye ameletwa nchini na Kampuni Bingwa ya Burudani hapa nchini Prime Time Promotions Ltd/Clouds Media Group na kudhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Limited kupitia kinywaji chake maalum cha Fiesta 2011, Serengeti Primeum Lager.

Post a Comment

0 Comments