Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Vijana Ajira na watu Wenye ulemavu Ridhiwani Kikwete akisalimiana na wajumbe nje ya ukumbi huo leo Tarehe 25 ,Aprili 2025.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (MB) amewataka viongozi hao kutobabaishwa na wanaopitapita kutafuta nafasi za uongozi kabla ya muda badala yake wawapuuze.
Dkt. Akson amesema uongozi hautafutwi kwa nguvu bali unapangwa na Mwenyezi Mungu
Wakati huohuo Mjumbe wa Kamati Kuu na Mlezi wa Mkoa wa Pwani Lailah Burhan Ngozi Mkoani Pwani ambaye alikua mgeni rasmi kwenye Mkutano Mkuu wa Jimbo la Kibaha Mjini wakati Mbunge wa Jimbo Silvestry Koka alipokuwa akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 - 2025.
Ngozi amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshirikiana vema na wabunge katika kuleta maendeleo na kumpongeza Mbunge Koka kwa kazi kubwa kwa kuutumia uongozi wake kwa maslahi mapana ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
" Tunahitaji Viongozi bora kwa kuzingatia misingi bora ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambayo inatoa majibu ya kuifanya iendelee kuwa Chama Kiongozi."amesema Ngozi.
Amesema kuwa CCM siyo chama goigoi bali ni chama chenye uwezo wa kutekeleza ahadi zake kwa vitendo.
Ngozi amesema kuwa wanaopinga maendeleo yaliyofanywa na Dkt. Samia Suluhu Hassan hawana sera hivyo wasiwapotezee muda.
"Msitafute wagombea wababaishaji nje ya CCM tafuteni viongozi wanaotokana na CCM kwani wao wamelelewa na wana maadili ya Kiuongozi." amesema Ngozi.
Amehitimisha kwa kuwataka viongozi wa mkutano huo kutosemeana maneno mabaya hususani kwa viongozi walioko madarakani.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge wakiteta jambo na Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa kupitia Kundi la Wazazi y Chama Cha Mapinduzi MNEC Hamoud Jumaa.




0 Comments