MAMLAKA YA HIFADHI YA NGORONGORO(NCAA) YASHIRIKI MAONESHO NA KONGAMANO LA UWEKEZAJI LA UTALII ZANZIBAR 2024

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) inashiriki Maonesho na Kongamano la Uwekezaji na Utalii linalofanyika tarehe 25 na 26 Oktoba 2024, Dimani, Fumba, Zanzibar. Katika maonyesho hayo, NCAA inatangaza fursa za uwekezaji katika miradi ya utalii na miundombinu ndani ya hifadhi. Vivutio vya kipekee kama Kreta ya Ngorongoro, Bonde la Olduvai, na Eneo la Ndutu vinavutia wawekezaji na kuimarisha nafasi ya Tanzania kwenye ramani ya utalii wa kimataifa.

NCAA pia inatoa elimu kwa washiriki kuhusu uhifadhi wa maliasili na umuhimu wa urithi wa dunia, ikiwahamasisha kuunga mkono uhifadhi shirikishi unaolenga kulinda na kuboresha mazingira ya hifadhi. Washiriki wanajifunza mikakati endelevu inayotekelezwa na NCAA ili kulinda maeneo haya muhimu.

Maonyesho haya ni jukwaa muhimu kwa NCAA kuwahamasisha wawekezaji kushirikiana nao katika miradi ya uhifadhi na utalii, ili kuchangia katika uchumi wa taifa na kuhakikisha kuwa urithi wa Tanzania unadumu kwa vizazi vijavyo.

Post a Comment

0 Comments