WASTARA HANA MAWAZO YA KUOLEWA KWA SASA

 Wastara akiwa na marehemu mume wake Juma Kilowoko 'Sajuki' enzi za uhai wao. 

MCHEZAJI Filamu nyota wa kike nchini  nchini, Wastara Juma  amesema anakutana na changamoto nyingi katika kuandaa filamu zake tangu alipofiwa na mume wake mpendwa, Sajuki Juma aliyekuwa msaada mkubwa kwake.
Sajuki alifariki Dunia Januari 2, 2013 katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa kwaajili ya matibabu akisumbuliwa na uvimbe pembeni ya ini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi, Wastara alisema, kutokana na kukutana na changamoto nyingi katika kazi zake, ameamua kutafuata meneja ambaye wanatasidiana.
“Tangu nimefiwa filamu ambazo nimefanya mwenyewe ni kama mbili tu, changamoto zilizopo kwangu ninafanya kazi peke yangu kazi zinakuwa nyingi na sina msaada,”.
“Nimeamua kumtafuta meneja ambaye atanisaidia baadhi ya kazi muhimu kwasababu watu wanahitaji kazi nzuri kwa hali hiyo imenilazimu nitafute mtu wa kusaidiana nae,” alisema.
Aidha, Wastara alikanusha uvumi wa kwamba amechumbiwa na kwamba bado anamkumbuka mumewe, Sajuki hivyo kwasasa hana mpango tena wa kuolewa labda hapo baadae.

Post a Comment

0 Comments