skip to main |
skip to sidebar
LULU AFIKISHA MIEZI NANE (8) MAHABUSU
KESI
ya mauaji inayomkabili msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael
(Lulu), dhidi ya aliyekuwa msanii mwenzake, Steven Kanumba, inaendelea
kupigwa kalenda kwa madai kwamba upelelezi haujakamilika.
Kesi hiyo
iliahirishwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya
Hakimu Mkazi, Augustino Mbando. “Mheshimiwa hakimu, upelelezi wa kesi
hii haujakamilika, tunaomba tarehe nyingine ya kutajwa,” alidai Wakili
wa Serikali, Kenneth Sekwao.
Hakimu Mbando alikubali kuahirisha kesi
hiyo hadi Desemba 17 mwaka huu, kwa ajili ya kutajwa. shitakiwa
anatetewa na mawakili, Kennedy Fungamtama, Peter Kibatara na Fulgence
Masawe.
Lulu yuko rumande kwa miezi nane sasa kutokana na makosa ya
mauaji na kukosa dhamana, anadaiwa kwamba Aprili 7 mwaka huu maeneo ya
Vatican, Sinza, alimuua Steven Kanumba.
Kuchelewa kukamilika kwa
upelelezi kumeanza kuzua mjadala kwa watu mbalimbali wanaofika
kusikiliza kesi hiyo, wakidai kwamba hawajui matukio gani nchini ambayo
upelelezi wake unaweza kufanywa kwa haraka.
“Nashindwa kuelewa, kila
siku upelelezi bado, kuna upelelezi gani katika kesi hii wa kumaliza
mwaka mzima, kila kesi ina mazingira yake ya kuchelewesha upelelezi
lakini hii…” alihoji msikilizaji huku akitoka katika chumba cha
mahakama.
No comments:
Post a Comment