Social Icons

Thursday, October 20, 2011

BELLE 9 GODZILLA KUPAMBA MISS UTALII DODOMA

Wasanii wa Musiki wa kizazi kipya wa R&B,Hip Hop Belle 9 na GodZilla,wanatarajiwa kuwa kivutio cha aina yake katika shindano la kumpata Miss Utalii Dodoma 2011/2012.Onesho hilo litakalo fanyika tarehe Jumamosi ya 29-10-2011 katika ukumbi wa Club La-Azziz Dodoma linataraji kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kiserikali wa mjini Dodoma na nje ya Dodoma.Hii inatokana na ukweli kwamba kwa muda mrefu kumekuwa na mvutano baina ya wanamuziki wa kizazi kipya wanao fanya Hip Hop na wale wanao fanya R& B,kila upande ukidai kuwa aina ya muziki wake iko juu kuliko nyingine. Belle 9 anapiga R& B wakati Godzilla anapiga Hip Hop hivyo kufanya usiku huo wa kumpata Miss Utalii Dodoma 2011/12 kuwa na mvuto na burudani ya aina yake,kwani pia kutakuwa na burudani ya ngoma za asili kutoka kwa kundi machachari la ngoma za asili la Yangeyange arts Group la mjini Dodoma.

Wasanii hao wa Muziki wa kizazi kipya na wale wa ngoma za asili wamekamiana pia kuonyesha kipi bora kati ya ngoma za asili na muziki wa kizazi kipya.

No comments:

 
 
Blogger Templates