Rais mstaafu wa awamu ya nne na mjumbe maalum wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amewasilisha ujumbe maalum kwa kiongozi wa Burki Faso Kepteni Ibrahim Traore Jijini Ouagadougou na kushuhudiwa na baadhi ya Maafisa Waandamizi wa nchi zote mbili.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt.Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Kiongozi wa Burkinafaso Kepteni Ibrahim Traore walipokutana leo tarehe 18 Aprili 2025 Jijini Ougadougue.Mhe. Kikwete amewasilisha salamu za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambazo zimeelezea umuhimu wa nchi za Afrika kuimarisha ushirikiano wa kijamii na kiuchumi kama njia muhimu kwa bara hilo ikiwa na lengo la kujitegemea, hususan katika kipindi hiki ambapo misaada kutoka nchi za magharibi imepungua kwa kiasi kikubwa.
Kiongozi wa Burkinafaso Kepteni Ibrahim Traore.







0 Comments