WAJUMBE KAMATI ZA MAADILI MAAFISA MAHAKAMA WAASWA KUISHI KIAPO CHAO

Mahakimu wa Mahakama  za Wilaya Mkoa wa Pwani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mhe.Jaji Mfawidhi Salma Magimbi.
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani alipomuwakilisha na kufungua mafunzo hayo ya siku moja.
Jaji  Mfawidhi Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam, Salma  Maghimbi ametoa wito  kwa Wajumbe  wa Kamati za Maadili   Maafisa  wa Mahakama Mkoa wa Pwani  kuishi kiapo chao walichoapa leo tarehe 25 Februari  2025.

"Nawasisitiza  mkaishi viapo vyenu mlivyo apa  pia nawashukuru kwa utayari wenu wa kuitikia kuwa kwenye Kamati hii" amesema Jaji Mfawidhi Maghimbi

Amesema kuwa Wajumbe wanapaswa kuwa na hofu ya Mungu kwa sababu kazi wanayokwenda kuifanya inahusiana na maisha ya watu.

"Tuko katika nguzo ya tatu ya mhimili wa nchi, hizo kamati zimeanzishwa kwa lengo  la kumsaidia mwananchi mwenye malalamiko yake ama kutoridhishwa na maamuzi ajue  wapi mahali sahihi  pa kupeleka malalamiko yake.

Kamati ya Mkoa  ya Maadili ya Maafisa  wa Mahakama inaundwa na Mkuu wa Mkoa husika ambaye  atakuwa Mwenyekiti, Hakimu mkazi mfawidhi wa mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa na Wajumbe  wengine  wawili watakao teuliwa  na Mkuu wa Mkoa kutoka miongoni mwa watu  mashuhuri  katika Mkoa , ambao  wana uadilifu wa hali ya juu, walio na ufahamu na uwezo ambao ni muhimu katika kushiriki  kikamilifu katika  utekelezaji  wenye  ufanisi wa majukumu ya Kamati pamoja na Maafisa wawili wa  Mahakama watakaoteuliwa na Jaji Mfawidhi

 Aidha Katibu wa Kamati  hiyo atakuwa  Mwanasheria  wa Serikali  Mfawidhi  katika Mikoa yenye ofisi ya Mwanasheria  Mkuu wa Serikali na katika Mikoa ambayo haina  Ofisi  ya Mwanasheria mkuu wa Serikali  Katibu atakuwa Katibu  Tawala wa  Mkoa.

"Majukumu ya Kamati  ni kupokea  na kuchunguza  malalamiko  yaliyowasilishwa na wajumbe wa umma kuhusiana  na Mahakimu  wa Wilaya  au Mahakimu Wakaazi  katika  Mkoa  husika  na Kisha  kuwasilisha ripoti Tume" amesema Jaji Mawidhi Maghimbi.

Amesema kuwa Kamati itatakiwa kufanya  uchunguzi  wa mwenendo wa Mahakimu  wa Wilaya  au Mahakimu  Wakaazi kwa kuzingatia  maelekezo  ya Jaji Mfawidhi na kutoa  ripoti kwake au kuchukua hatua  muafaka kulingana  na Sheria.

"Kutekeleza  majukumu mengine kadiri ambavyo Jaji Mkuu anaweza kwa maandishi ya mkono wake  kuelekeza kwa Mwenyekiti" amesema Jaji Mfawidhi Maghimbi. 
Mahakimu wa Mahakama  za Wilaya Mkoa wa Pwani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mhe.Jaji Mfawidhi Salma Magimbi.
Mkuu wa Wilaya Petro Magoti ambaye ameapishwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kisarawe  akizungumza  jambo kwenye mafunzo hayo.

Post a Comment

0 Comments