MH. IDDI AZZAN AZINDUA KAMPENI JIMBO LA KINONDONI JIJINI DAR

 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge (kushoto) akimtambulisha Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CCM, Mh. Iddi Azzan(kulia) mbele ya umati wa wanachama wa chama hicho na wananchi waliofurika katika viwanja vya  CCM Mwinjuma Mwananyamala jana jioni.a , wakati wa uzinduzi wa kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, katika jimbo hilo, jijini Dar es Salaam.(Picha na Geofrey Adroph waPamoja blog)
Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CCM, Mh. Iddi Azzan akizungumza na wananchama na wananchi wa maeneo mbalimbali ya jimbo la Kinondoni waliofurika katika viwanja vya  CCM Mwinjuma Mwananyamala jana jioni wakati wa uzinduzi wa kampeni
 Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akihutubia umma uliohudhuria uzinduzi wa kampeni za mgombea ubunge jimbo la Kinondoni kupitia tiketi ya CCM.
 Meya mstaafu wa Manispaa ya Kinondoni, Salum Londa akimwaga sera za CCM mbele ya umati wa wanachama wa chama hicho na wananchi waliofurika wakati wa ufunguzi wa kampeni za mgombea ubunge jimbo la Kinondoni zilizofanyika waliofurika katika viwanja vya  CCM Mwinjuma Mwananyamala jana jioni.
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge akiwasalimia pamoja na kutoa neno kwa wananchama na wananchi waliofika kwenye mkutano huo wa ufunguzi rasmi wa kampeni za mgembea Ubunge jimbo la  Kinondoni .
Mgombea udiwani kata ya Mwananyamala Bw. Songoro Mnyonge(kushoto) akitambulishwa kwa wananchi na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge(kulia)
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge  akimtambulisha Mgombea udiwani wa kata ya Kijitonyama,  Ndg. Kamugisha wakati wa ufunguzi wa kampeni za Mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni
Mgombea udiwani kata ya Tandale Bw Tamimu akitema vidonge kwa wapinzani.
Bw. Massawe ambaye ni mgombea udiwani kata ya Ndugumbi akizungumza jambo wakati wa mkutano huo
 Mgombea Udiwani kata ya Magomeni Ndugu Bujugo akiwaomba kura wananchi waliofika kwenye mkutano huo na pia kuwapigia wabunge pamoja na raisi kupitia chama cha CCM
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge (kushoto) akipokea kadi ya CUF toka kwa bibi  ambaye alikuwa ni kada wa chama hicho alidai hajaona manufaa yeyote kuwepo katika chama hicho ambapo alijitoa rasmi na kurudi CCM.
Bibi akiwasalimia wananchama na wananchi waliofika kwenye mkutano huo
Mzee Dalali akihutubia mamia ya watu waliohudhuria mkutano huo ambao mwenyewe alidai umati ulifikia watu laki 250.
Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CCM, Mh. Iddi Azzan akiendelea kumwaga sera
Umati mkubwa ukishangilia wakati wa mkutano

Baadhi ya wananchi waliofika kwenye mkutano huo


Wasanii wa kizazi kipya Tundaman na Bonge la Nyau wakitumbuiza mara baada ya Mkutani kwisha
Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CCM, Mh. Iddi Azzan akiaga mashabiki wake baada ya kumaliza kuhutubia katika viwanja vya  CCM Mwinjuma Mwananyamala jana jioni.

NA KHADIJA KALILI
MGOMBEA wa Jimbo la Kinondoni Iddi Azzan anayegombea kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi amewaambia wakazi wa Kinondoni kwamba watasahau adha za mafuriko kwa sababu zipo fedha kutoka Benki ya Dunia ambazo zitafanya kazi ya kuchimba na kuupanua mto  Ng’ombe  na mto Msimbazi.
Alikwenda mbali kwa kusema kwamba pesa ya fidia ya nyumba ambazo zitavunjwa ili kupisha upanuaji wa mito hiyo ziko hivyo wanasubiri utekelezaji .
Alisema kwamba anajivunia kwa kuweza kuusafisha mto Ng’ombe ambao ndiyo umekuwa chanzo cha kuleta mamfuriko kutokana na wakazi wa waliojenga pembeni ya mto huo kutupa takataka hovyo.
Azzan alisema hayo katika uzinduzi wa kampeni zake uliofanyika jumapili kwenye uwanja wa CCM mwinjuma Mwananyamala Jijini Dare es Salaam.
Aidha aliongeza kwa kusema kuwa serikali imetenga kiasi cha fedha ambapo kila kata itapata  sh.mil 100 ambazo zitatumika kwa ajili ya mikopo nafuu  zitakazosaidia  kinamama , vijana ili waweze kujiajiri.
Aidha alisema kwamba endapo wananchi watamchagua na kurudi tena madarakani atahakikisha wafanyabiashara wa Kinondoni ambao ni mama lishe, baba lishe , bodaboda na wamachinga wengine waweze kufanya biashara zao bila kubughudhiwa huku wakiwekewa utaratibu maalum.
“Machinga wote watawekewa utaratibu  mzuri ambao  utawasaidia  kufanya biashara zao vizuri” alisema Azzan.
Naye Mstahiki Meya wa Kinondoni Yusuph Mwenda aliposimama kumuombea kura Azzan aliwasisitiza wakazi waliojitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi huo kumchagua Azzan kwa sababu ni mchapakazi .
“Tumesafisha sana mito ya Ng’ombe, Tandale ikiwa ni katika kupambana na mafuriko licha ya changamoto kubwa ni utupaji wa taka hovyo unaofanywa na wakazi hivyo mpigieni kura ili aweze kuleta maendeleo zaidi na kutengeneza mazingira mazuri ya mito na maeneo mbalimbali ya Kinondoni” alisema Mwenda.
Wakatohuphuo Azzan alisema kwamba yeye kama Mbunge  kabla muda wake haujamaliza aliweza kuketi na uongozi wa Manispaa ya Kinondoni na kuunda sheria ndogondogo ikiwemo ya tika ambayo itawahusu wakazi wa jimbo hilo watatakiwa kulipa kiasi cha sh.50,000 kwajili ya Bima ya afya ambapo mtu akilipia atatibiwa kwa muda wa mwaka mmoja.
Azzan amewaahidi wakazi wa kinondoni kuboresha zaidi afya ikiwemo hospitali ya Mkoa wa Mwananyama na hospitali zingine na wilaya kama Tandale na Sinza.
Pia aliahidi kujenga wodi za watoto wsachanga na
“Hivyo ili mpango huu uweze kutimia chagueni Iddi Azzan kwa maendeleo na afya zenu kwa ujumla” alisema Azzan.
Azzan anawania kiti hicho kwa tiketi ya CCM ambapo tayari aliweza kushikilia kwa miaka 10 iliyopita.

Post a Comment

0 Comments