Social Icons

Friday, October 22, 2010

DK GHARIB BILALI AMKUMBUKA MAMA MARIA NYERERE

Mama Maria Nyerere akizungumza na Dk. Gharib Bilali.
Mama Maria Nyerere akizungumza na Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, wakati Dk Bilal alipofika nyumbani kwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere leo okt 21 kwa ajili ya kumsalimia Mama Maria Nyerere. (Picha zote na Muhidin Sufiani).
Mgombea mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Mama Maria Nyerere, wakati alipofika nyumbani kwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere eneo la Mwitongo Kijiji cha Butiama.
Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akiongozana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Makongoro Nyerere wakati alipofika Eneo la Mwitongo Kijiji cha Butiama, nyumbani kwa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa ajili ya kumsalimia Mama Maria Nyerere jana Okt 21.


No comments:

 
 
Blogger Templates