Social Icons

Thursday, October 21, 2010

MWISHO KUANGUSHIWA BONGE LA PATI IJUMAA CLUB CONTINENTAL

Mwisho Mwampamba kesho Ijumaa asubuhi atakuwa na mkutano na waandishi wa habari utakaofanyika katika hoteli ya Holiday Inn na baadaye usiku litaangushwa bonge la Party ya kumkaribisha nyumbani katika Club Continental iliyopo Mtaa wa Nkrumah kati kati ya jiji la Dar es Salaam. Hiyo ni kumpongeza kwa kuingia katika fainali za shindano la Big Brother Africa All Stars ikiwa ni mara ya pili mfululizo.Itakumbukwa mwaka jana Mtanzania Richard Bezuideihout aliibuka mshindi hivyo siyo vibaya kwa mshiriki wa mwaka huu kukosa lakini amewakilisha na anastahili pongezi.Blog hii inakuahidi kukuletea kila litakalojiri katika viunga hivyo.

No comments:

 
 
Blogger Templates