MCHENGERWA AIPONGEZA NMB KUHAMASISHA KUPANDA MITI MASHULENI

Mwonekano wa miti iliyopandwa na wanafunzi wa Sekondari ya Shule ya Mwambisi Forest iliyopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, akikabidhi hundi ya shilingi milioni 50 kwa mwalimu wa shule ya Sekondari Mwambisi Forest wakati wa hafla iliyofanyika kwenye shule hiyo iliyopo wilayani Kibaha Mkoani Pwani, mara baada ya shule hiyo kuibuka washindi wa shindano la upandaji miti shuleni.

Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI ,Mohammed Mchengerwa amesema kuwa ameipongeza Benki ya NMB kwa kuhamasisha zoezi la upandaji miti katika Shule za Msingi na Sekondari nchini.

Waziri Mchengerwa ametoa maelekezo kwa Wakuu wa Wilaya , Makatibu Tawala,Wakurugenzi na Wakuu wa Mikoa yote nchinikuhakikisha wanaendeleza na kusimamia upandaji wa miti na kuhakikisha inakua , tekelezeni suala la upandaji wa miti 1,500 katika kila Halmashauri zote nchini na zoezi hilo litakuwa moja ya kipimo cha uwajibikaji kwani bila miti hakuna binaadamu.

Nawapongeza sana Benki ya NMB kwa kulijali taifa lao kwa kupanda miti wamekua mfano bora kati ya sekta binafsi na sekta ya umma,hata katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM inasisitiza upandani wa miti na utunzaji wa mazingira.

"Mimi kama mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa nimefurahishwa kwa Wilaya Kibaha kuongoza katika shindano hilo hongereni sana Mkoa wa Pwani pia nawapongeza sana NMB kampeni hii haikuishia Tanzania Bara bali imefika hadi Visiwani Zanzibar yaliyofanyika (Tarehe 12,Aprili 2025) yatachochea kuibua kizazi cha vijana wenye mtazamo mpya katika utunzaji mazingira"

Mkurugenzi wa Fedha Benki ya NMB  Juma Kimori  akizungumza  kwenye hafla hiyo.

"Maelekezo ya Makamu wa Rais ni Sheria maelekezo aliyotoa kwa Mamalaka ya Serikali za Mitaa ni amri msingi wake ni utekelezaji tutakapokuwa tunapita huko katika Halmashauri tutahitaji kuona inatekelezwa, Naibu Katibu Mkuu wandikie Halmashauri zote kuwa zoezi hili ni endelevu la upandaji wa miti kwa moyo wa dhati nawapongeza washiriki wote walioshiriki na kushinda kupanda miti na kukua katika kiwango cha 99% hii inaonesha kuwa ninyi ni vijana wasikivu na wema wenu nahitaji niuone katika matokeo yenu ya kidato cha nne na cha sita na nitawafuatilia", amesema Mchengerwa.

"Nawapongeza Benki ya NMB kwa kutoa uamuzi wa kutenga Mil.225 kwa ajili ya zawadi ya motisha kwa shule zilizopanda miti ambazo zimetolewa leo"amesema  Mchengerwa. 

Mchengerwa amesema hayo tarehe 12 Aprili 2025 alipokuwa mgeni rasmi kwenye tukio la kukabidhi zawadi kwa washindi wa Kampeni ya Miti Milioni 'Kuza mti Tukutunze' hafla iliyofanyika katika viwanja vya Sekondari ya Mwambisi Forest Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.

Shule ya Sekondari ya Mwambisi Forest iliyopo Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani imeibuka kinara kwa kupanda miti 2,000 ambayo imetunzwa kukua kwa kiwango cha 99% , kwa ushindi huo wamezawadiwa hundi yenye thamani ya Mi.50

Nafasi ya pili imekwenda kwa Shule ya Ibondo kutoka Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza ambao wamepata hundi ya Mil. 30 nafasi ya tatu imekwenda kwa Shule ya Msingi Itimbo Sekondari wamepata hundi ya Mil.20

Mchengerwa amewaomba Benki ya NMB waendelee kuchangia maendeleo ya nchi katika kushirikiana kwenye nyanja mbalimbali za maendeleo nchini.

Akizungumza kwa Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Pwani Seka Urio alikaribisha wageni na kutambulisha wahudhuriaji kwenye hafla hiyo,huku wengine waliohudhuria ni pamoja na Katibu Mkuu TAMISEMI Adolf Ndunguru, Kamishna wa Uhifadhi Wakala wa Misitu Tanzania Prof. Dos Santos, Afisa Mkuu wa Fedha Juma Kimori, Katibu Tawala Mkoa wa Pwani (RAS) Rashid Mchatta , Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon,Naibu Waziri OR-TAMISEMI (Afya) John Dugange.

Zoezi la upoandaji miti 1500 kila Mkoa lilizinduliwa mwaka 2023 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango kwenye Mji wa Kiserikali Mtumba Dodoma.

Post a Comment

0 Comments