Social Icons

Tuesday, August 16, 2016

UJIO WA MRS LUCY IWE CHACHU KATIKA SANAA




Baadhi ya matukio katika igizo la Mama Lucy anakwenda Afrika (Mrs. Lucy goes to Africa)  likiwa limeigizwa na Msanii kutoka Marekani Bi Toussaint Duchess lililofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Agosti 15 . Picha na Raymond Mushumbusi


Mkurugenzi  wa Idara ya habari (MAELEZO)  Hassan Abbas amesema kuwa ujio wa msanii wa maigizo kutoka nchini Marekani   Toussaint Duchess maarufu kama ‘Mrs. Lucy’ ulete chachu katika amendeleo ya sanaa  kwa wadau wake hapa nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Nape Nnauye aliyekuwa mgeni rasmi  kwenye  uzinduzi wa igizo la  Mrs. Lucy linaloitwa ‘Mrs. Lucy Goest to Africa’  Abbas alisema kuwa ni vyema  wadau wa sanaa wakatumia ujio huo kama changamoto itakayowasaidia kujifunza na kuwa  wabunifu zaidi katika kazi zao za sanaa.

“Ujio wa muigizaji Mrs. Lucy ni changamoto kwa wadau wa sanaa nchini, ni fursa ya kujifunza kwa wasanii hususani katika eneo la sanaa za jukwaani, vile vile ni fursa kwa vijana wa kitanzania ambao wanatarajia kufanya kazi  za sanaa” Abbas.

Bongoweekend  ambayo ilikuwepo  kwenye onyesho hilo  lililofanyika kwenye ukumbi  hapo  iliweza kushuhudia  wadau mbalimbali wakifurahia   kutokana na wasanii wa hapa nyumbani kuweza kumudu vyema  katika uchezaji  wa maigizo kana kwamba walikuwa wakicheza  mtu wa kawaida na siyo yule msanii nyota Mrs. Lucy kutoka nchini Marekani.

Wasanii ambao wa nyumbani waliong’ara ni pamoja na  mama na mwana  waliojikita muda mrefu kwenye  tasnia ya filamu na maigio ambao ni Suzan Lewis (Natasha) na binti yake Yvone Cherry  (Monalisa)ambao wameshiriki  na kuonesha ubunifu na umahiri wa hali ya juu  ikiwa ni pamoja nha kumleta nchini msanii huyo.

Aidha Abbas  ametoa pongezi kwa kituo cha televisheni cha Azam na wasanii   Natasha na Monalisa ambao wameshiriki  kwa ubunifu wa kumleta msanii huyo nchini pamoja na maboresho mengine yaliyoofanywa na Azam.

Azam TV  wanatarajia kuonyesha igizo hilo la msanii huyo kutoka nchini   pamoja na filamu mbalimbali zitakazofanywa na msanii huyo.

No comments:

 
 
Blogger Templates