Mkurugenzi wa EAGGroup Imani Kajula (Kushoto) akifafanua jambo katika mkutano huo jana akifuatiwa na Rais
wa Klabu ya Simba, Evans Aveva, akifuatiwa na Meneja Mawasiliano ya Kibiashara wa Tigo Jacqueline Nnunduma wakati walipozungumza na waandishi wa habari, Dar es
Salaam wakati wa uzinduzi wa huduma ya Simba News kupitia Simu za mkononi
za Tigo, ambapo mteja atajiunga kwa kuandika neno SIMBA kwenda namba 15460,
kisha kukatwa sh. 150 kwa siku.
KWA mara nyingine tena Klabu
ya Simba
wamezindu huduma ya kuwapasha habari mashabiki wake kwa kupitia simu za
mkononi itakayofahamika kwa jina la ‘Simba News’.
Akizungumza jana katika mkutano
na waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es Salaam Rais wa klabu hiyo
Evance Aveva alisema kwamba Simba watashirikiana na Kampuni ta Tigo katika
kuhakikisha mashabiki wake wanapata
taarifa za timu yao.
“Huu ni mwanzo hivyo mashabiki
wakae mkao mzuri kwani mambo mengi mazuri yanakuja kwa sababu tuko katika hatua
za mwisho na Kampuni zingine za simu ambao nao watakuwa wakitoa huduma kama hii
ili kuweza kuwafikia mashabiki wetu kwenye mitandao yote” alisema Aveva.
Aveva aliongeza kusema anampongeza Mkurugenzi wa Kampuni ya EAGGroup
Imani Kajula ambao ni wasimamizi wakuu wa tovuti ya klabu hiyo pia wamekuwa ni washirika wao katika upande wa
kibiashara kwa kuweza kuwa wabunifu katika
kuiwezesha Simba ikijingaza kitaifa na Kimataifa pia uwepo wao ndani ya
Simba kumeleta tija.
Mkurugenzi wa EAGGroup Imani Kajula aliongeza kwa kusema kuwa wao wanatambua umuhimu wa kutoa taarifa hivyo wameanza na Tigo kwa huduma ya Simba Sms ambayo itagharimu kiasi cha sh. 150 tu huku akitoa wito kwa mashabiki kujiunga na huduma hiyo ili waweze kupata taarifa za timu yao.Ili kujiunga shabiki atatakiwa kuandika neno SIMBA kwenda 15460.
No comments:
Post a Comment