Social Icons

Thursday, May 21, 2015

USAJILI WARSHA YA UANDISHI WA FILAMU FUPI ZIFF

WARSHA nyingine ya uandishi wa filamu inatarajiwa kufanyika wakati wa tamasha la Majahazi la ZIFF litakalofanyika Julai mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Daniel Nyalusi,  ilisema warsha hiyo itaendeshwa tena na Maisha Lab ya Uganda.
Alisema maombi kwa wanaotaka kushiriki yameanza kupokewa na mwisho ni Juni 13.
Nyalusi alisema warsha za Maisha Lab, zimekuza vipaji vya waandishi wa filamu na wakurugenzi wa filamu wengi Afrika Mashariki.
“Wanaotaka kusaidiwa katika hili wanatakiwa kufika ZIFF, Ngome Kongwe Zanzibar, au kutuma maombi yao ya kusaidiwa kwa barua pepe workshop@ziff.or.tz,” alisema Nyalusi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Maisha Lab, Fibby Kioria, alisema wanatarajia kutoa ‘scholarship’ 60 kwa mwaka kwa washiriki kutoka nchi zote za Afrika Mashariki, nia ikiwa ni kuongeza ujuzi na kupanua wigo wa biashara ya utengenezaji wa filamu.
Alisema katika kila warsha, ‘script’ zitashindanishwa na mshindi atapata dola 5,000 za Marekani ili kumwezesha kutengeneza filamu fupi katika mwaka unaofuata.
Mwaka jana, Nassir Qassimwa kutoka Tanzania ndiye aliyeibuka mshindi.

No comments:

 
 
Blogger Templates