Social Icons

Friday, November 28, 2014

MHESHIMIWA PROF. ANNA TIBAIJUKA BORA UJIUZULU KULINDA HESHIMA YAKO NA CHAMA

PROFESA ANNA TIBAIJUKA.

Na Projectus Ishengoma Lugumalila

MHESHIMIWA Bi.Anna Tibaijuka (MB) Waziri wa Ardhi ni moja wa viongozi wachache sana wenye ujasiri na kiongozi muwazi katika sakata zima la Tageta ESCROWkwani kiongozi huyu amekiri wazi kuwa amepokea fedha Billion 1.6 kutoka kwa mmiliki
wa Kampuni ya VIP Engineering Bw.James Rugemalira tena si fedha ndogo.
Si jambo jema kumuhukumu Mheshimiwa Anna Tibaijuka lakini siyo vibaya kumshauri kwa kuwa amekuwa muwazi katika sakata hili,basi lingekuwa jambo la maana sana kama angejiuzulu madaraka aliyonayo katika serikali ili kulinda heshima yake na ya chama tawala Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Msomi yoyote yule anapofikia kuitwa Profesa na tena Waziri mwenye kushika dhamana ya nchi na wananchi yaani Ardhi na makazi, ardhi ndio kila kitu kwa
Watanzania, halafu akafikia sehemu ya kukubali kupokea fedha ya kiasi kikubwa Sh. Billion 1.6 kutoka kwa mfanyibiashara ! naye Mhe.Anna Tibaijuka bila ya kutia shaka yoyote kama ananunuliwa kwa namna moja au nyingine kutokana na dhamana ya cheo chake? hapa kwa Mtanzania yoyote haingii akilini.

Litakuwa jambo bora kwa Mhe.Anna Tibaijuka kujiuzulu ili aonyeshe mfano bora kuwa yeye ni Kiongozi mkweli na Viongozi wengine watafuata nyayo.

Tunajua mtu anapoitwa Profesa siyo msomi wa kawaida bali msomi aliefikia daraja la juu kabisa,ndiyo maana tunaona msomi kama kiongozi wetu huyu ambaye anajua wazi kuwa yeye ni mmojawapo wa Mawaziri wachache ambao Wizara zao
zina dhamana kubwa ya nchi, leo hii anakubali kununuliwa kiurahisi pia kufanya biashara akiwa katika madaraka mazito,kama ataendelea kututumikia wananchi katika Wizara ambayo pia inahusika na mipaka ya ardhi ya nchi,tuna mashaka nae.

Watanzania tunajiuliza hivi  Tibaijuka yupo katika utumishi wa umma tena katika Wizara muhimu na huku akiwa Mkurugenzi wa Mashirika au shule na miradi binafsi au? ndiyo kusema cheo chake cha utumishi wa umma ndio dhamana ya biashara zake ?
Hivi kuna hosptali ngapi hapa nchini hazina dawa?  je wakina mama wangapi wajawazito wanafariki wakati wa kujifungua kwa ukosefu wa vifaa vya mahosptalini? Shule ngapi ? za serikali ambazo hazina madawati?

Leo Mheshimiwa ambaye tena ni Profa amepokea fedha Sh.Billion 1.6 na kusema kuwa hakujua kama ni fedha chafu, watanzania tunamashaka nae.

"Profesa Tibaijuka anafahamu wazi kuwa amevunja sheria ya maadili ya viongozi wa umma 
(Sheria namba13 ya mwaka 1995)  ambayo inawataka viongozi watoe taarifa ya zawadi wanazopokea au malipo wanayolipwa".

Sisi wananchi wenye kuiamini serikali hii na juhudi za Kiongozi wetu Mhe.Rais Dkt. Jakaya Kikwete (Mungu amuongezee afya njema), hatuwezi kabisa kukubali au kuona kiongozi tena msomi Profesa ,anavunja dhamana ya wananchi na kumvunjia heshima mkuu wa nchi ambaye ndiye alikuteuwa.

Litakuwa jambo la busara sana Tibaijuka ujiuzulu ili kulinda heshima yako kama msomi Profesa ,pia kulinda heshima serikali na chama tawala.

Huwezi kutumikia ofisi mbili utumishi wa umma na biashara. Wanachi tunasikitika sana kuona katika sakata la fedha za umma mpaka baadhi  ya watumishi wa mungu ambao ni viongozi wa Kanisa nao wanahusika na bila ya uwoga wanapokea fedha bila ya hofu ya kujenga udini.
Mungu ibariki Tanzania,Mungu mzidishie afya njema kiongozi wetu Raisi  Kikwete .

No comments:

 
 
Blogger Templates