Social Icons

Friday, December 9, 2011

TAFAKURI YANGU KATIKA KUSHEREHEKEA MIAKA 50 YA UHURU

 
Wadau Nawatakia Heri ya Miaka 50 ya Uhuru  nimechelewa lakini namshukuru mungu  kuiona siku ya leo na nina imani kila kitu kimekwenda sawa jambo moja kubwa ni kwamba ni ukweli usiopingika miongoni mwetu  watanganyika wengi ambao sasa ni Watanzania  hatutaweza kuiona miaka mingine 50  na kuisherehekea kama ilivyokuwa  hivyo ni vyema tujiulize umeifanyika nini ardhi ya Mama Tanganyika kabla ya kutoa lawama , je tumetangaza  vema utalii wetu na kutumia ipasavyo / inavyotakikana  ardhi katika nyanja ya kilimo , madini, mito , bahari, na kuchapa kazi ipasavyo ikiwa ni katika kutafuta maendeleo yako wewe binafsi, familia yako na taifa zima kwa ujumla nasema hivyo kwa sababu hata katika vitabu vya dini wameandika ipende dunia na kujiwekea mazingira mazuri ya kuishi kama  vile utaishi milele na itafute ahera kama utakufa sasa hivi hilo ndilo neno langu la leo mwenye macho haambiwi tazama. 
KILA LA KHERI WATANZANIA WOTE POPOTE PALE MLIPO KATIKA KUMBUKUMBU YA SIKU MUHIMU AMBAYO NCHI YETU ILIPATA UHURU WAKE KUTOKA KWA MKOLONI MUINGEREZA.

1 comment:

Anonymous said...

mavazi kama hayo uliyovaa kwenye picha hapo juu janakupendeza sana. unaweza ukapata mume kwa hayo.

 
 
Blogger Templates