Social Icons

Tuesday, April 19, 2011

MAKAMU WA RAIS DKT.GHARIB BILAL ATIA SAINI KITABU CHA RAMBIRAMBI UBALOZI WA BRAZIL NCHINI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akisaini katika kitabu cha rambirambi wakati alipofika kwenye Ofisi za Ubalozi wa Brazil nchini, kuweka saini katika kitabu hicho maalum kutokana na kifo cha Makamu wa Rais wa zamani wa nchi hiyo,Jose Alencar da Silva, aliyefariki dunia hivi karibuni..(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais). Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kushoto) akizungumza na Balozi wa Brazil nchini, Francisco Soares Carlos Luz, wakati Makamu alipofika kwenye Ofisi za ubalozi huo Dar es Salaam jana, kwa ajili ya kutia saini katika kitabu cha rambirambi cha aliyekuwa Makamu wa rais wa zamani wa Brazil, Jose Alencar da Silva, aliyefariki hivi karibuni nchini humo. Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais.

No comments:

 
 
Blogger Templates