Social Icons

Saturday, October 23, 2010

Z-ANTO:MIPANGO MINGI YA MAISHA YANGU ILIKWAMISHWA NA MWANAMKE

Hatimaye kijana aliyefanya vizuri na ngoma kadhaa miaka michache iliyopita, Ally Mohamed Ahmad a.k.a Z-Anto amefunguka na kupiga stori mbili tatu na ShowBiz zikiwemo ishu zinazohusu maisha yake ya ndani.Akisema na safu hii kwa njia ya simu kutoka pande za Kigamboni, msanii huyo ambaye hivi sasa amerudi upya na ngoma yenye jina la Kisima cha malavidavi alitamka kwamba mipango mingi aliyokuwa nayo katika maisha yake ilivurugwa na msichana ambaye yeye humuita mtoto wa kike bila kumtaja jina lake.“Kwa mfano hivi sasa baada ya kuwa peke yangu nimefanikiwa kufungua saluni huku kwetu Kigamboni iitwayo ‘Kwetu salon’ mipango ambayo nilikuwa nayo kitambo ila mtoto wa kike niliyekuwa naye akanivurugia malengo. Kwa sasa nina kila sababu ya kusema asante Mola kwani jina langu linarudi na biashara zangu zinakwenda kama nilivyotarajia, ‘i am back’,” alisema Z-Anto(Chanzo Abby Cool na Ijumaa ShowBizz)

No comments:

 
 
Blogger Templates