Social Icons

Thursday, November 16, 2017

CHUO KIKUU MZUMBE WAMUENZI BABA WA TAIFA HAYATI MWL. JULIUS KAMBARAGE NYERERE KWA KONGAMANO

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Prof. Lughano Kusiluka, akitoa hotuba yake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika Mdahalo wa Kumbukizi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uliofanyika jana katika ukumbi wa Samora uliopo Chuo Kikuu cha Mzumbe Kampasi ya Morogoro. Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa mtazamo wa Mwl. Nyerere juu ya uongozi na menejimenti kwa minajili ya kuleta maendeleo. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Laurian Ndumbaro akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Mdahalo wa Kumbukizi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uliofanyoika katika Chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro jana. Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa mtazamo wa Mwl. Nyerere juu ya uongozi na menejimenti kwa minajili ya kuleta maendeleo. Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Prof. Ganka Nyamsogoro, akitoa hotuba ya kumshukuru mgeni rasmi. Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa mtazamo wa Mwl. Nyerere juu ya uongozi na menejimenti kwa minajili ya kuleta maendeleo.[/ Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani). Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa mtazamo wa Mwl. Nyerere juu ya uongozi na menejimenti kwa minajili ya kuleta maendeleo. Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Rainfrida Ngatunga (kulia), akifuatilia mada katika mdahalo wa Kumbukizi ya Mwalimu Julius Nyerere uliofanyika jana katika ukumbi wa Samora uliopo Chuo Kikuu cha Mzumbe Kampasi ya Morogoro. Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa mtazamo wa Mwl. Nyerere juu ya uongozi na menejimenti kwa minajili ya kuleta maendeleo.
Prof. Justin Kalisti Urassa, akitoa mada juu ya sera ya viwanda katika Kumbukizi ya Mwalimu Nyerere iliyofanyika jana katika ukumbi wa Samora uliopo Chuo Kikuu cha Mzumbe Kampasi ya Morogoro. Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa mtazamo wa Mwl. Nyerere juu ya uongozi na menejimenti kwa minajili ya kuleta maendeleo. Mmoja wa washiririki wa mdahalo wa Kumbukizi ya Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa ameshika kitabu kuhusu Uongozi na hatima ya nchi yetu. Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa mtazamo wa Mwl. Nyerere juu ya uongozi na menejimenti kwa minajili ya kuleta maendeleo. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Laurian Ndumbaro (kulia), akibadilishana mawazo na Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Sylvia Lupembe na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Prof. Lughano Kusiluka. Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa mtazamo wa Mwl. Nyerere juu ya uongozi na menejimenti kwa minajili ya kuleta maendeleo Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Mzumbe, Prof. Mathew Luhanga, akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Laurian Ndumbaro (kulia) na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Prof. Lughano Kusiluka. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Laurian Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na waandaaji wa
mdahalo wa Kumbukizi ya Mwalimu Julius Nyerere. (Picha na: MAELEZO)

No comments:

 
 
Blogger Templates