Social Icons

Friday, February 10, 2017

SHAMRASHAMRA ZA TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA ZANZIBAR

Mwenyekiti wa Tamasha la Busara Zanzibar Simai Mohammed Said akiwa na Mabalozi wa Norway na Uswisi kutoka kushoyo    ni Balozi wa Uswisi Tanzania Balozi Florence Tinguely na Balozi wa Norway Tanzania Balozi Hanne Marie wakiangalia wakiangalia vikundi vya Utamaduni wakati wa Uzinduzi wa Tamasha la Sauti za Busara katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisongo  wakiangalia burudani hizo.
Wasanii wa Kikundi cha Utamaduni kutoka Nchini Burundi wakitoa burudani kwa  wakazi  wa Zanzibar katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michenzani Zanzibar kabla ya kuanza kwa maandamano ya uzinduzi huo ulioanzia katika viwanja hivyo hadi  viwanja vya bustani ya forodhani.
Wasanii kutoka burundi wakionesha umahiri wao wa kupiga ngoma za utamaduni wa Kwao. 


Wananchi waliofika katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michenzani wakifuatilia burudani za wasanii mbalimbali kabla ya kuaza kwa maandamano ya ufunguzi wa Tamasha la Busara Zanzibar.
Mwenyekiti wa Tamasha la Sauti za Busara Zanzibar akitoa maelezo kwa Mabalozi wa Uswisi na Norway walipokuwa katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu wakipata maelezo ya Mnara huo

Kikundi cha Six Unity wakionesha umahiri wao wa kujenza Dance wakati wa uzinduzi huo katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michenzani.
Wasanii wakitoa burudani katika Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michenzani Kisonge.
Wanafunzi wa Skuli ya Maandalizi Jangombe wakicheza ngoma ya Bomo katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu kabla ya kuanza kwa maandamano ya uzinduzi wa Tamasha la Busara Zanzibar.


Wananchi wakifuatilia burudani zilikuwa zikitolewa  na vikundi mbalimbali vya utamaduni vinavyoshiriki Tamasha la Busara Zanzibar.

Imeandaliwa na OthmanMapara.

Zanzinews.com.
othmanmaulid@gmail.com.

No comments:

 
 
Blogger Templates