skip to main |
skip to sidebar
MISS KANDA MASHARIKI VIPAJI KUFANYIKA IDD PILI MAISHA PLUS KIBAHA
Baadhi ya washiriki wa shindano hilo wakiwa katika picha ya pamoja.
WAREMBO
14 wanaowania taji la Kanda ya Mashariki ‘Redds Miss Eastern Zone 2014’ watashindania taji la vipaji ‘Talent Award’
lililopangwa kufanyika siku ya Idd Pili kwenye ukumbi wa Maisha Plus (Police
Mess) Kibaha, Mkoa wa Pwani.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa
mashindano hayo, Alex Nikitas alisema kuwa kutokana na mashindano hayo ya
vipaji, kambi ya warembo iliyopangwa kuanza Julai 29 kwenye hotel ya Usambara
Safari Lodge, sasa itaanza Julai 28 kwenye hotel ya Precision mkoani Pwani.
Nikitas
alisema kuwa maandalizi ya mashindano hayo yamekwisha kamilika na warembo hao
mbali ya kushindana katika vipaji, pia watatoa msaada kwa kituo cha watoto
yatima cha mkoa wa Pwani na baadaye kurejea mkoani Morogoro tayari kwa
mashindano yaliyopangwa kufanyika katika
hoteli ya Nashera Hotel Agosti 8.
Alisema
kuwa mashindano hayo yatashirikisha jumla ya warembo 14 kutoka mikoa minne
ambayo ni Pwani, Lindi, Mtwara na mwenyeji, Mkoa wa Morogoro chini ya udhamini
wa Redds Original, Zanzi Cream Liquer, Pepsi, Usambara Safari Lodge, Kitwe
General Traders, Starwing Lodge, Nashera Hotel, CXC Africa, Sykes Travel, Sasa
Saloon, Grand Villa Hotel, Shabibby Line na Clouds FM.
Nikitas
anawataja warembo hao kuwa ni Lucy Julius Diu, Prisca Mengi, Tarchisia
Noback Mtui na Angel Shio ambao wanatoka Morogoro. Warembo wengine ni Elizabeth
Tarimo, Lilian Andrew na Leila Abdul Ally ambao wanatoka mkoa wa Lindi ambapo
kutoka Mtwara ni Nidah Fred Katunzi, Lightness Mziray na Nelabo Emmanuel.
Pia
warembo kutoka Pwani ni Khadija Ramadhan Sihaba, Irene Rajabu Soka, Mary Mpelo
na Arafa Shaban. Nikitas alisema kuwa warembo hao watakuwa kambini kuanzia
Julai 29 kwenye hotel ya Usambara Safari Lodge chini ya Miss Kanda ya mashariki
mwaka jana, Diana Laizer.
No comments:
Post a Comment