Social Icons

Thursday, July 31, 2014

MFALE WA NYIMBO ZA ASILI COSTA SIBOKA KUPAMBA MISS MWANZA

MSANII  anyetamba kwa nyimbo za asili  nchini Costa Siboka ‘Mfalme’  au unaweza kumwita ‘Mwana Ukerewe’ anatarajia kupamba katika onyesho la kumtafuta Miss Mwanza  2014.Akizungumza katika ofisi za Tanzania Daima jana  Siboka alisema  shindano hilo limepangwa kufanyika Agosti 8 mwaka huu kwenye ukumbiulioko katika hoteli ya nyota tano ya Gold Crest.

“Katika shindano hilo nitaonyesha shoo yangu mpya inayokwenda kwa jina la ‘Engele yange’  maana yake ni samaki wangu  ambao nimeuimba katika lugha ya Kikerewe” alisema.

Kadhalika ameweka vionjo vya lugha ya Kisukuma ‘Nakutogile’ likiwa na maana ya Nakupenda.
Aidha pia ametunga wimbo wa Kihaya ambao unakwenda kwa jina  la ‘Otandekela Bojo ‘ (Usiniache).
Vile vile anao wimbo mwingine aliouimba katika lugha ya Kikurya ‘Omuisike’ (Binti ambaye bado hajaolewa ama mwali).
Siboka ametamba na nyimbo za ‘Niwewange’ (wewe ni wangu ) ambapo alipiga katika mtindo wa ‘Wawawa’, ‘Ndelule’ ambayo ni lugha ya Kinyamwezi huchezwa katika msimu wa mavuno napia huimbwa kwa mashujaa wa uwindaji wanaporudi kutoka porini.
Pia Siboka aliwahi kutwaa taji la watunisha misuli wa Mkoa wa Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla na kuiwakilisha nchi katika michuano ya Afrika iliyofanyika nchini Misri ambako alitunukiwa Diploma ya kutunisha misuli na Rais wa Africa Body Building Federation  (AFBB).
Baada ya hapo Siboka ataendela na ziara ya kutambulisha nyimbo zake  mpya katika ziara  ya mikoa ya kanda ya ziwa iliyodhaminiwa na kinywaji cha wakulima Balimi Extra Lager na Kampuni ya CXC Africa.

No comments:

 
 
Blogger Templates