Social Icons

Saturday, April 5, 2014

SHINDANO LA KUSAKA VIPAJI VYA KUIGIZA TANZANIA LAENDELEA VIZURI, WENGI WAHAMASIKA NA KUJITOKEZA KWA WINGI


Vijana waliojitokeza kwaajili ya kushiriki shindano la kusaka vipaji vya Kuigiza wakiingia katika eneo la Ukumbi wa Isamilo lodge tayari kwa kuanza kuonyesha Vipaji vyao
Baadhi ya vijana wakijaza fomu kwaajili ya kuja kuonyesha vipaji vyao katika shindano la kusaka vipaji Tanzania ambalo linaendelea kufanyika katika Ukumbi wa Isamilo Lodge
Mmoja wa Majaji wa Shindano la Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents, Ivon Chery akitabasamu mwara baada ya kufurahishwa na Mmoja wa Washiriki wa shindano la kusaka vipaji (hayupo pichani) wakati alipofika mbele kuonyesha kipaji chake.
Majaji wakiwa Kazini Kutoka Kulia Ni Single Mtambalike, Ivon Chery na Roy Sarungi.
Cresenciah Helman akiwa mbele ya Majaji wa Shindano la Kusaka vipaji vya Uigizaji Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents akisikiliza kwa makini maelezo ya Majaji wakati alipofika kwaajili ya kuonyesha Kipaji chake leo kwenye ukumbi wa Isamilo lodge.
Kijana akionyesha Kipaji mbele ya Majaji.
Akiwa mbele Ya Meza ya Majaji.
Mmoja wa washiriki, Cresenciah Helman akishukuru timu ya Majaji baada ya kufurahishwa na uwezo wake wakati alipofika kuonyesha kipaji chake cha kuigiza leo katika Ukumbi wa Isamilo lodge.
Vijana wakiwa katika harakati za kujaza fomu kwaajili ya kuonyesha vipaji vya kuigiza katika shindano la kusaka vipaji vya uigizaji Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents linaloendelea Katika Ukumbi wa Isamilo Lodge.Picha na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

No comments:

 
 
Blogger Templates