Social Icons

Wednesday, August 28, 2013

FLORA MBASHA KUZINDUA INUA MOYO WANGU MNAMO TRH 15 SEPT 2013


Tamasha la uzinnduzi wa album hii mpya kufanyika mnamo Tarehe 15/09/2013 katika uwanja wa Kawe pale Tanganyika Peckaz.

Flora Mbasha ataimba live nyimbo zake zote kuanzia album ya Jipe Moyo hadi ya sasa.
Siku hiyo tukio lote litarekodiwa live katika video.

Hatua hii imekuja ikiwa ni katika harakati zake za utumishi wa Mungu kupitia kipaji chake cha uimbaji muziki wa Injili, ambapo mwanamuziki huyu mahiri wa kimataifa amepania kwa mara nyingine tena kuonyesha jinsi gani anavyoweza kuwashika wapenzi wa muziki wa injili. 

Ni album iliojaa 'Utatu mtakatifu', album ambayo inadhihirisha ni namna gani Flora Mbasha na timu inayomzunguka anavyotumia vyema kipawa chake kumtukuza na kumwabudu Mungu aliye hai.

Eh banaeeee....!!! 
TIMUA MBIO UINASE KOPI YAKO KWA MARA YA KWANZA PALE UWANJANI.
MUNGU AKUBARIKI. 

No comments:

 
 
Blogger Templates