Social Icons

Wednesday, June 6, 2012

RAIS KIKWETE ACHANGIA BILIONI 3.2 KATIKA HARAMBEE YA KUCANGIA MKAPA HIV/AIDS FOUNDATION

 Rais Jakaya Kikwete, akimkabidhi picha ya kuchora Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya UNDI Consulting Group Limited, Bw Philip Makoka aliyoinunua kwa shilingi milioni 20 wakati wa Harambee ya kuchangia fedha programu ya Mkapa Fellows inayoendeshwa naTaasisi ya Mkapa HIV/AIDS iliyofanyika Dar es Salaam kwenye hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency jijini Dar es salaam. Kulia ni mchoraji wa picha hiyo, Bwana Muzu
                                                               (PICHA NA IKULU).
  Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Bw. Deo Mwanyika, Makamu wa Rais wa Kampuni ya Barrick Tanzania baada ya kuibuka mchangiaji mkubwa kwa kutoa dola za Kimarekani laki 5 kwa ajili ya kuchangia taasisi ya Mkapa Hiv/Aids Foundation Jumanne Juni 5, 2012 usiku katika hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam. Kushoto ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa aliyeandaa hafla hiyo iliyoweza kukusanya shilingi bilioni 3.2 na kuvuka malengo ya harambee hiyo kwa asilimia sita

 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi (kushoto) na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa baada ya kuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia Taasisi ya Mkapa HIV/AIDS foundation na kusaidia kukusanya shilingi bilioni 3.2 nauvuka malengo ya harambee hiyo kwa asilimia sita

No comments:

 
 
Blogger Templates