Social Icons

Saturday, April 2, 2011

WATAKAO CHAKACHUA TIKETI ZA SIMBA Vs MAZEMBE KUKIONA

Wakati tiketi kwa ajili ya kwenda kushuhudia mechi ya marudiano baina ya Simba na TP Mazembe yenye maskani yake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), utakaopigwa kesho Jumapili zikianza kuuzwa tangu jana, uongozi wa Simba umesema utawachukuia hatua kali na za kisheria kwa watu ambao watajaribu kughushi tiketi hizo. Taarifa zilizopatikana toka ndani ya Klabu hiyo yenye makao makuu yake mitaa ya Msimbazi zimewasisiza mashabiki kununua tiketi halali kwani kutakuwa na uhakiki na ulinzi wa hali ya juu wa tiketi siku ya pambano hilo.

No comments:

 
 
Blogger Templates