Social Icons

Friday, January 30, 2015

ASHA BARAKA ALLY CHOKI WAMALIZA BIFU LAO


MKURUGENZI wa Kampuni ya The African Stars Entertainment (ASET),Asha Baraka na Mkurgenzi wa bendi ya Extra Bango Ally Choki, leo wamemaliza tofauti zao katika ofisi za Global Publishers zilizopo Sinza Bamaga Jijini Dar es salaam.

Akizungumza na Tanzania Daima Asha alikiri kwamba habari hizo ni za kweli na kwa sasa yeye na Choki hakuna chuki kati yao.

Wadau mbalimbali walitoa maoni yao katika mtandao na kutoa ushauri kama ifuatavyo kwa wakurugenzi hawa.

Mirinda Nyeusi ambaye kwa sasa yuko nchini Duabi kikazi alisema kwamba anasifu waili hao kumaliza bifu walilokuwa nao kwa miaka kadhaa kwani halisaidii kitu chochote  ila ni kujivunjia njia ya mungu.

“Safi sana mama wanamuziki wote wa Tanzania pamoja na Prezident Mzee wa Farasi” alisema Mirinda.Huku Mzee Yusuf akisema neno moja tu Alhamdulillah.

Naye Karima Chichi Mhandeni amabye ni mdau wa muziki wa dansi nchini alisema laiti kama angelikuwa akitumia kilevi basi leo angekunywa kwa furaha kwani chuki siyo nzuri  hata mungu hapendi  na hakuna jambo lisiloisha mungu awajaalie awaepushe na shari  za dunia kwani wao ni wamoja na wanategemeana , kuna leo na kesho  hajui atakayemuokota mwenzie tunashukuru.

 Kwani tunahitaji  tuone kazi  na sio  tofauti, hii hadithi inanifundisha  kuwa watu wagombanao ndiyo wapatanao .

Aidha Mwenyekuvunja undugu hataona pepo sisi sote  ni ndugu , mungu awajaalie

Wakati huohuo Lulu Kiluvia aalisema “Nisha kutana na watu hawawezagi kuweka kitu kinyongo hua Asha baraka namba  moja mtatofautiana lakini ipo siku kwake yataisha sasa kazi kwenu mnao kuaga wapambe nuksi “ alisema Kiluvia.

Choki na Asha Tumefurahi sana kuwaona mpo pamoja hili ni tukio zuri hata vitabu vya dini vinasema patana na nduguyo maana hujui muda wala saa ambayo mungu atakuhitaji , mwenye kuupenda muziki wetu wa dansi hii ni habari njema sana kila mmoja hapo anatambua umuhimu wa mwenzake  Choki anajua ametangaza namna gani jina lake kupitia bendi hiyo lakini kama sikosei yeye ndiye ameshiriki album nyingi na zilizofanya vizuri sana hapo hayo Asha lazima ayakumbuke hao watu wana mengi ya kuwafanya waheshimiane washikamane ili zoezi linaloendelea la kuupigania muziki huu liwe na nguvu moja.

“Ally  najua unanijua naitwa Championi niko  Mtwara mi nashukuru saana kwa tendo  hilo  wote wewe na dada Asha mmefuata  dini inavyotaka  nimefurahi sana rudi twanga tujenge bendi Choki”.

Maoni yaliyotolea ni mengi kama vile wasanii ni kioo cha jamii hivyo wasimame katika mema na umoja na ushirikiano vilevile ustahamilivu ili wengine wajifunze toka kwao Mashabiki tusiingilie ugomvi wa wamiliki na wanamuziki, kwetu Sisi tunachohitaji ni amani na burudani.
Choki  na Asha walikuwa mahasimu bada ya Choki kuihama Twanga na kwenda kuanzisha bendi yake  hadi kufikia kiasi cha kutopeana salamu na kuapizana wasizikane  pindi mmoja kati yao atakapokufa.

No comments:

 
 
Blogger Templates