Social Icons

Thursday, August 22, 2013

MAALIM GURUMO ATANGAZA RASMI KUSTAAFU KUIMBA ,MUZIKI

 Wadau wakipiga picha na Maalim Gurumo

KAMANDA na gwiji wa muziki wa dansi katika bendi ya Msondo Maalim Muhidin Gurumo (73) ametangaza  kuacha rasmi kujighulisha  muziki wa dansi kama jinsi aliyoifanya kwa muda wa miaka 53.

Gurumo aliyasema hayo  leo saa sita mchana  katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO Dar es Salaam.

“ Leo nimekuja kuwaga  rasmi wanamuziki na wapenda muziki na waliokuwa mashabiki wangu  kwa ujumla , sitaki tena muziki ila ikumbukwe kwamba muziki  ni asili yangu  ila  sasa nimeamua kustaafu  kwa moyo mmoja hivyo naahidi kuwa nitawasaidia  wanamuziki wanaobaki kwa uhuru na moyo mmoja” alisema Gurumo. ), jijini

Wakati huohuo, Gurumo anasema anastaafu akiwa hana kitu cha maana katika tasnia ya muziki wa dansi licha ya kuutumikia na kufanya kazi kwa moyo wake wote  kwa kipindi cha miaka 53 iliyopita.

“Nilianza kuimba nikiwa  kijana wa umri wa miaka 20  mwaka 1960 na tangu hapo sikuwahi kubadili kazi lakini sasa nastaafu ilhali nikiwa sina hata baiskeli” alisema Gurumo.

Wakati huohuo Mratibu mkongwe nchini wa matamasha mbalimbali na muanzilishi wav iota na  kumbi nyingi za burudani hapa jijini Dra es Salaam Juma Mbizo anatajwa na Gurumo kuwa ndiye atakuwa mratibu katika tamasha maalum litakaloandaliwa la kumuaga .

Katika kamati hiyo pia wamo,  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya The African Stars Entertainment ‘Aset’ Asha Baraka, Mdau wa burudani Said Mdoe, Richardson Sakalla, Mkurugenzi wa bendi ya  The Kilimanjaro  ‘Wana Njenje’ Waziri Ally.

“Hii kamati imeundwa ili  ili iweze  kumsaidia  katika kumuandalia tamasha maalum , hivyo ipo siku tutaweka  wazi tumeandaa kumfanyia nini  mkongwe huyu  wa dansi kadhalika siku hiyo ya tamasha lake ndipo atakapoimba kwa mara ya mwisho na kuanzia leo  hatopanda katika jukwaa lolote kuimba” alisema 

Mbizo aliongeza kwa kusema kuwa Gurumo amepata ridhaa kutoka kwa wanamuziki wenzake wote  kabla kufikia uamuzi huo wa kustaafu muziki na kwakuwa ameimba kwa miaka mingi  sasa mi wakati wake wa kupumzika.

Wosia wake kwa wanamuziki wanao baki anasema yeye anawaasa wapige muziki wa nyumbani  hasa waliokuwa wakipiga bendi ya Msondo “Wapige muziki ambao tulikuwa tunapiga sisi zamani  tofauti na hivi sasa ambapo wanamuziki na vijana wengi wanakimbilia katika muzikiwa Bongo Fleva ambao ni muziki unaokwenda na wakati lakini ni  wa kupita.
 Mwisho anamalizia kwa kusema kwamba  kustaafu kwake hakuzuii yeye kutoa ushauri au kufundisha wanamuziki na wapiga ala kwani anakipaji cha kumfundisha mpigaji wa chombo chochote kwa kutumia mdomo wake.

Kadhalika Gurumo anasema kwamba katika nyimbo alizowahi kuimba wimbo anaoupenda ni wimbo wa ‘Usimchezee  Chatu’ ambao aliumba kipande kidogo mbele ya  Waandishi wa Habari na katika wanamuziki wa Bogo Fleva anampenda Naseeb Abdul ‘Diamond’.                                                                                                                             


Gwiji Maalim Gurumo aliyekaa katikati, kushoto ni Meneja wa Bendi ya Msondo Kibiriti na Mratibu wa tamasha Juma Mbizo.Waliosimama ni waandishi wa habari Khadija  na Hemed Kivuyo (ITV).Hapa ni mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo.

No comments:

 
 
Blogger Templates