Social Icons

Sunday, October 22, 2017

UWT MKOA WA DAR ES SALAAM WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA MAFANIKIO YA MAZUNGUMZO NA BARRICK GOLD MINE.


Mwenyekit wa  Umoja wa wanawake Tanzania ( UWT ) mkoa wa Dar es salaam Mama Janeth Masaburi aliye nyoosha mkono juu  akiimba wimbo na wanawake wa umoja huo  katika maandalizi ya kutoa tamko la umoja huo  mkutano ulio fanyika ilala Jijini Dar es salaam ( na John Luhende wa  Mwambawa habari)


 Wanacha wa UWT mkoa wa Dar nes salaam wakicheza wimbo wa CCM mbelekwa mbele katika kumpongeza mwenyekiti wa chamama Cha  Mapinduzi CCM, Dr John Pombe Magufuli ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzaia .


Wanawake wa umoja wa wanawake  Tanzania (UWT)  mkoa wa Dar es salaam, wakisikiliza tamko la umoja wao likisomwa na Mwenye kiti wao Mama Janeth Masaburi.( na John Luhende wa  Mwambawa habari)

Na John Luhende . 
Umoja wa wanawake wa Tanzania UWT  Mkoa wa Dar es salaam , umempongeza Rais wa jamhuri ya Muungano Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kwa kufikia makubaliano ya na kampuni ya ya uchimbaji madini ya Dhahabu ya balick  Gold mine na kumtaka kuendelea  na hatua hiyo kwa ulinzi wa lasilimali za taifa  kwaajili ya vizazi vijavyo.

Akisoma tamko hilo  mwenyekiti wa UWT  Mkoa wa Dar es salaam ,Janeth Masaburi, amesema ,hatua hiyo ni ushindi dhidi ya wapinga Maendeleo,na kusema kuwa kutokana na hatu anazo zichukua  mhe. Rais Magufuli nidhahiri kuwa kunabaadhi miongoni mwa watanzania watabeza hatua hizo lakini nivema wakapuuziwa na kuwakitu kimoja ili tuweze kushinda vita hivi vya kiiuchumi.

Aidha amesema makubaliano hayo yaliyofikiwa yanatija na faida kwa Taifa na watanzania kwa kutoa ajira na mazingira bora ya kazi tofauti na hapo awali ambapofaida ya madini hayo ilikuwa inaishi kwa makampuni ya wageni.
Pamoja na hayo Mama Masaburi amesema ,  umoja huo huo umemwomba kushugulikia pia na madini aina ya Urenium na joto ardhi ili nayo yaweze kunufaisha Taifa.

No comments:

 
 
Blogger Templates