Social Icons

Wednesday, August 30, 2017

BONDIA IDDI MKWELA ASEMA KAMOTE NA MFAUME MFAUME WANANIKIMBIA


Na Mwandishi Wetu


BONDIA Idd Mkwela baada ya kumsambalatisha bila ya huruma bondia Adam Ngange hivi karibuni amekuwa katika wakati mgumu wa kupata mapambano zaidi kwa kuwa mabondia wa nchini kwa sasa wanamkimbia

mana mpaka sasa nimepewa ofa ya kupambana na mabondia wawili tofauti ambao wananiogopa na naisi wameingia mitini kwa kipigo nilichotoa kwa Ngange

Mkwela alikwenda mbali zaidi na kuwataja mabondia Allan Kamote kutoka Tanga na bondia anaetamba kwa sasa Mfaume Mfaume kuwa wananikimbia kwa kuwa kazi yangu ninayo onesha nikiwa ulingoni ni zaidi yao hivyo nawaonya wakae wakijua siku nikikutana nao ama zao ama zangu

Mkwela anaenolewa na Sako Mwaisege 'Dungu' nae ametilia mkwazo kwa kuwataka mabondia hawo ambao kwa sasa awana tambo mbele ya mkwela kwani Mkwela ni moto wa kuotea mbali ata hivyo izo kazi zilikuja katika kambi yetu mara gafla tukasikia zimepeperuka yani wametukimbia

hata hivyo atuchoki tunaendelea kufanya mazoezi najua ipo siku wataingia katika anga zetu kwani awana ujanja wa kunikwepa bali wanachelewesha kupigana na sisi

Kocha Mwaisege aliongeza kwa kusema kuwa Mkwela katika viwango vya ubora nchini Tanzania kupitia mtandao wa Boxrec anashikilia namba mbili baada ya bingwa wa Dunia wa GBC  Ibrahimu Class 'King Class Mawe' hivyo najua watakuja tu kwa kuwa mimi ndio nipo juu zaidi yao

ukimwangalia Kamote yeye ni namba kumi na mbili hivyo nimempita mbali sana ana ujanja na sasa amechoka ngumi zimekwisha na sasa ni zamu yangu mimi kutamba akuna wa kuuzima moto wangu katika uzito wa lightweight kg 61  mimi ndie mtawala wa uzito huo hivyo wajipange sana vinginevyo wabadilishe uzito ili kujiepusha na kipigo nitakacho wapa alimaliza kusema Mkwela

No comments:

 
 
Blogger Templates