Social Icons

Friday, June 16, 2017

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA SULUHU HASSANI AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA JIJINI DAR ES SALAAAM

 Watoto wakikimbia walipokuwa wakiandamana kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kinyerezi, ambapo yalifanyika kimkoa wilayani Ilala, Dar es Salaam leo.Maadhimisho hayo yaliongozwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan. PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Maandamano yalielekea kwenye viwanja hivyo
 Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akiwashukuru na kuwapatia vyeti wauguzi wa kujitolea  walioshiriki kampeni kupima magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa watoto na vijana  wakati wa T
 WATOTO WAKIPIMWA UREFU
 Maandamano
 Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akiwasalimia watoto pacha Brighton na Bright Shirima alipokuwa akikagua mabanda ya tiba kwenye Tamasha la Uelimishaji na Upimaji Afya na Kinga dhidi ya Magonjwa yasiyoambukiza kwa watoto na vijana wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika
 Kikundi cha hamasa cha Ilala kikihamasisha wakati wa maadhimisho hayo
 Brass Band ya Polisi ikiongoza maandamano 
 Makamu wa Rais Samia akisalimiana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kigwangala
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akihutubia 

 Kikundi cha ngoma cha Shule ya Msingi Umoja kikitumbuiza kwa ngoma ya kibati wakati wa maadhimisho hayo

 Kikundi cha Umoja kikitumbuiza kwa ngoma ya Makhirikhiri


 Makamu wa Rais, Samia akimkabidhi cheti cha shukrani DkNg'wege aliyekuwa mmoja wa madaktari walioshiriki kupma afya za watoto na vijana wakati wa maadhimisho hayo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akihutubia katika maadhimisho hayo.Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigangwala na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi kote nchi kuwafichua watu wanaonyanyasa na kudhalilisha watoto kijinsia ili waweze kukamatwa na kuchukua hatua za kisheria kama hatua ya kukomesha vitendo hivyo ambayo vimeanza kushamiri katika baadhi ya jamii nchini.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa agizo hilo katika hotuba yake ya kuhitimisha kampeni ya kudhibiti magonjwa yasiyo ya kuambukiza ambayo ilitoa huduma bure za vipimo na matibabu kwa watoto na vijana zaidi ya 1500 kampeni ambayo iliambatana na maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika katika viwanja vya Shule ya msingi Kinyerezi mkoani Dar es Salaam.

Makamu wa Rais amesema kuwa watenda maovu hao lazima vifichuliwe na wananchi, walezi pamoja na wazazi kwa kuwa watu wanaofanya vitendo hivyo vya udhalilishaji wa watoto wapo miongoni mwa jamii.

Katika kukabiliana na hali hiyo, Makamu wa Rais ameviagiza vyombo vya dola kutofumbua macho vitendo hivyo bali pindi wanapopata taarifa za matukio ya udhalilishaji wa watoto wachukue hatua za haraka za kuwakamata na kuwachukulia hatua stahiki watu wanaofanya vitendo hivyo vibaya.

Makamu wa Rais pia ametoa wito maalum kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kote nchini waache kuwaficha watu wanaotendea vitendo hivyo vibaya bali wawapatie taarifa walimu wao na polisi ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Amesema kwa kufanya hivyo watoto watakuwa salama katika mazingira ya nyumbani na wakiwa mashuleni kwani watu wabaya wanaofanya vitendo hivyo watawajibishwa kulingana na matendo maovu waliyokuwa wanawafanyia watoto hao.

“Mtoto anaweza kufaidika na fursa sawa iwapo tu atalindwa kwa kuwezeshwa kuwa afya bora”, Amesisitiza Makamu wa Rais.

Kuhusu kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema magonjwa yasiyo ya kuambukiza yameendelea kuua watu kwa kasi katika nchi zinazoendelea Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania.

Amesema ipo haja ya kuimarisha juhudi za kukabiliana na tatizo hilo kwa ushirikiano wa wadau wote kwani janga hilo linagharimu taifa na wananchi wake wakiwemo watu wazima, watoto na vijana.

“Magonjwa yasiyo ya kuambukiza yasipodhibitiwa yatapunguza uzalishaji mali,ufanisi mahali pa kazi na hata shughuli za ulinzi na usalama nchini mwetu na hivyo pato la taifa litapungua na taifa kuwa watu maskini kutokana na magonjwa hayo”, Alifafanua Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kuwa katika kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza Serikali imeweza kupanua maeneo ya kutolea huduma kwa wagonjwa wa saratani nchini kwa kujenga jengo jipya katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road na kuongeza majengo mapya ya huduma za saratani kwenye Hospitali za Rufaa ya kanda ya Bugando mkoani Mwanza.

Amesema Serikali pia imejenga Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ambayo ni taasisi ya mfano ya kutibu maradhi ya moyo ambapo kutokana na kujengwa kwa taasisi hiyo Serikali imefanikiwa kuokoa mabilioni ya fedha ambayo yangetumika kuwagharamia wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Hamisi Kingwangala amemhakikishia Makamu wa Raia kuwa Wizara hiyo itaendelea kuweka mipango na mikakati imara ya kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza nchini.

Dkt Kingwangala ameomba wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za kidini na wadau wengine kushirikiana na Wizara ya Afya katika kuongeza kasi ya kukabiliana na magonjwa hayo ili yasiendelee kuteketeza maisha ya watu nchini

No comments:

 
 
Blogger Templates