Social Icons

Friday, May 12, 2017

KAMPUNI YA TANCOQL ENERGY YATEKELEZA AGIZO LA SERIKALI


Meneja Udhibiti Ubora wa Makaa ya Mawe wa Kampuni ya Tancoal Energy Tanzania Limited Bw. Bosco Mabena akielezea moja ya majukumu wayafanyayo katika Kitengo cha Udhibiti Ubora wa makaa ya mawe  yanayochimbwa kutoka mgodi wa makaa hayo uliopo Ngaka, Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma 10 Mei, 2017.


Baadhi ya Malori katika eneo la Kitai Wilayani Mbinga, Mkoani Ruvuma yakiwa yamepakiwa makaa ya mawe yakifungwa maturubai kwa ajili ya kuzuia makaa ya mawe hayo kunyeshewa na mvua ikiwemo kuchafuliwa na aina yoyote ya uchafu wakati wa kuyasafirisha makaa hayo 10 Mei, 2017.


Lori lililopakia makaa ya mawe katika eneo la Kitai Wilayani Mbinga, Mkoani Ruvuma likipimwa uzito kabla ya kwenda kufungwa turubai tayari kwa kuanza safari ya kupeleka makaa hayo kwa mteja wake, 10 Mei, 2017.


Naibu Meneja wa Mgodi wa Kampuni ya Tancoal Energy Limited (wa pili kulia) Bw. Edward Mwanga, Meneja Udhibiti Ubora wa Makaa ya Mawe wa Kampuni ya Tancoal Energy Tanzania Limited Bw. Bosco Mabena (wa pili kushoto), Afisa Mauzo na Usafirishaji wa Kampuni ya Tancoal Energy Tanzania Limited, Bi. Leahkissa Mwangosi pamoja na Meneja Mawasiliano Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) (kulia) wakielekea katika eneo la mzani wa kupimia malori katika eneo la Kitai Wilayani Mbinga, Mkoani Ruvuma 10 Mei, 2017.

No comments:

 
 
Blogger Templates