Social Icons

Tuesday, May 23, 2017

BONANZA LA KWAYA ZA VIJANA KUTOKA KWAYA MBALIMBALI LAFANA JIJINI DAR ES SALAAM

Kikosi cha kwaya ya Usharika wa Mabibo (waliovaa jezi za Dark Blue) na kwaya ya Usharika wa Kinondoni (waliovaa jezi nyekundu) wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mechi kuanza
Mpira ukiwa unaendelea ambapo kwaya ya Kinondoni waliibuka kuwa washindi
Baadhi ya wanakwaya pamoja na watumishi wa Sharika mbalimbali za Moravian jijini Dar wakiwa wanatazama Mpira
Mchezo wa Netball ukiendelea ambapo walikuwa wanacheza kwaya ya Usharika wa Mabibo na Uhuru ambapo kwaya ya Mabibo waliibuka washindi.
Kwaya ya Amani kutoka Usharika wa Mabibo wakifurahia ushindi baada ya kuibuka Videdea kwenye mchezo wa netball
Mpambano mwengine uliokuwa wakukata na shoka kati ya Kwaya ya Usharika wa Uhuru na Mabibo ambapo Mabibo waliibuka washindi
Hapa ni mashindano ya kukimbia kwa wanawake
Mashindano ya kukimbia kwa wanaume hapa watu walichomoka balaa
Hapa ilikuwa ni mashindano ya kukimbia na majunia ambapo ngoma ilikuwa nzito kweli lakini walioweza waliibuka kidedea
Hapa ilikuwa sasa kufukuza kuku ambapo baada ya purukushani akapatikana mshindi ambaye ndiye anaonekana hapo akifurahi.
Mshindi wa Kukimbiza Kuku Bw. Lewis kutoka Usharika wa Kinondoni akiwa amekabidhiwa zawadi yake ya Kuku.
Mshindi wa kukimbia na Majunia Bi. Emmy kutoka Usharika wa Uhuru akikabidhiwa nishani yake na katibu wa kwaya ya vijana kutoka usharika wa Mabibo.
Huyu dogo anaitwa Afsa ndiye aliibuka mshindi wa riadha kwa upande wa wanawake
Mshindi kwa kukimbiza upepo kwa upande wa wanaume Adam ajichukua zawadi yake
Washindi wa Mpira wa Miguu kutoka Usharika wa Kinondoni wakikabidhiwa kombe lao
Kwaya ya vijana kutoka Usharika wa Mabibo wakikabidhiwa kombe lao baada ya kuibuka washindi katika mchezo wa Netball

Picha zote na Fredy Njeje

No comments:

 
 
Blogger Templates