Social Icons

Tuesday, April 25, 2017

TBL YQZINDUA KAMPENI YA 'CASTLE LITE UNLOCKS' JIJINI DAR ES SALAAM

 Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),  Idara ya Kuunganisha Wateja Afrika Mashariki, George Kavishe (kulia), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati wa uzinduzi wa kampeni ijulikanayo, ‘Castle Lite Unlocks’. Kushoto ni Meneja Chapa Msaidizi wa Bia Laini Tanzania, Isaria Kilewo na katikati ni Meneja Masoko wa TBL Kitengo cha Bia Laini Afrika Mashariki, Amou Majok.


 Meneja Masoko wa TBL Kitengo cha Bia Laini Afrika Mashariki, Amou Majok (katikati), akizungumza kwenye mkutano huo.
 Mkutano ukiendelea.
 Waandishi wa habari wakiwa katika uzinduzi huo.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
 Wadau wakibadilishana mawazo katika mkutano huo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.


Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya kutengeneza Bia  Tanzania (TBL)) leo imezindua kampeni ijulikanayo, ‘Castle Lite Unlocks’ ambayo lengo lake ni kuhamasisha wateja wake wa bia chapa Castle Lite kuifurahia zaidi na pia kuwaleta pamoja katika tamasha kubwa litalofanyika mwezi wa Julai mwaka huu.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika katika ofisi za TBL zilizoko Masaki, Meneja Masoko wa TBL Idara ya Kuunganisha Wateja Afrika Mashariki, George Kavishe, alisema TBL kwa miaka imekuwa ikijikita katika kuwafurahisha na kuwachangamsha wateja wake, hasa vijana kwa matamasha ikiwemo muziki ambao upo katika vipaumbele vya kampuni hiyo.   

“Uzinduzi huu utafikia kilele chake tarehe 22 mwezi wa Julai mwaka huu ambapo kutakuwa na tamasha kubwa Dar es Salaam litakalowapa nafasi wateja wetu kushuhudia wanamuziki wakubwa wa ndani na nje ya nchi, hivyo kuwapa wateja burudani itakayokuwa kwenye kumbukumbu zao kwa muda mrefu”, alisema Kavishe.   

Kavishe aliongeza kuwa kwa kipindi hicho cha miezi mitatu ya kampeni, zawadi kedekede zitatolewa zikiwemo muda wa maongezi wa simu za mkononi wa zaidi ya milioni 30 na pia tiketi zaidi ya elfu moja kwa washindi wa droo ambazo zitakuwa zinashindanishwa.

Aliongeza kwamba bajeti ya kampeni nzima ni zaidi ya shilingi milioni mia saba.

Naye Meneja Masoko wa TBL Kitengo cha Bia Laini Afrika Mashariki, Amou Majok alisema kuwa TBL ina utaratibu mahsusi wa kuandaa matamasha mara kwa mara ili kuwashukuru wateja wake kwa kuwapa burudani na kuwahamasisha kuzifurahia vinywaji vyake ambavyo ni vya hali ya juu na vyenye ubora zaidi.   

No comments:

 
 
Blogger Templates