Social Icons

Thursday, December 22, 2016

SERIKALI YAIPONGEZA TAASISI YA NAMAINGO KUGAWA MRADI WA SUNGURA

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Namaingo Business Agency, Bi Ubwa Ibrahim akihutubia wakati wa uzinduzi wa kugawa miradi ya sungura kwa wajasiriamali eneo la Majohe, Dar es Salaam
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Namaingo Business Agency, Bi Ubwa Ibrahim akielezea jinsi mradi wa sungura utakavyowanufaisha wanachama wa kampuni hiyo wakati wa uzinduzi wa kugawa miradi ya sungura kwa vikundi vya wajasiriamali eneo la Majohe, Dar es Salaa. Anayesikiliza kushoto ni Mgeni rasmi ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, Donald Bombo. Jumla ya sungura 600 waligawiwa kwa wanachama wa Namaingo.

Azingumza kwa niaba ya Serikali, Mkurugenzi huyo kutoka Ofisi ya Rais, Bombo  alimpongeza Bi Ubwa kwa ujasiri na uthubutu alionao wa kuanzisha miradi mbalimba inayosaidia kuwanufaisha wananchi na kuinua vipato vyao. Aliahidi kuwa serikali itakuwa bega kwa bega naye kuhakikisha mipango ya kusaidia kiuchumi wananchi inafanikiwa.(PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Rabbit Republic mwanzilishi wa ufugaji wa sungura kutoka Kenya, Moses Mutua akielezea mipango yake ya kuzanzisha machinjio makubwa ya kisasa ya sungura hapa nchini.Jana vikundi 20 vya wajasiriamali viligawiwaq sungura ambapo kila kikundi kilipata sungura 27 wa kike na madume matatu.
 Mutua akionesha sungura wa mradi ambao ameiuzia Kampuni ya Namaingo kwa ajili ya miradi ya wajasiriamali. Nyama ya sungura itakuwa inauzwa nje ya nchi ambapo kila siku itauzwa tani 2.
 Bi Ubwa akiwa na mmoja wa wanachama wakicheza muziki kwa furaha wakati wa hafla hiyo
 Msanii akitumbuiza wakati wa hafla ya uzinduzi wa  ugawaji sungura
 Baadhi ya wajasiramali wakicheza muziki
 Wajasiriamali wakisikiliza kwa makini wakati Mkurugenzi wa Namaingo akihutubia

 Mmoja wa viongozi kutokaOfisi za Namaingo mikoani akitoa ushuhuda wa miradi waliyonayo na wanayotarajia kuianzisha.

Sehemu ya magari ya wajasiriamali waliofika katika uzinduzi wa miradi ya wajasiriamali

No comments:

 
 
Blogger Templates